ZAIDI YA ASILIMIA 90%YA MADEREVA PIKIPIKI AWANA LESENI

Mkijua sheria za usalama barabarani hata rushwa hamtatoa maana unajua sheria
Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha Marson mwakyoma akiongea na baadhi ya madereva wa pikipiki waliofuata pikipiki zao kituoni hapa ambazo zimekamatwa
ZAIDI ya  asilimia 90%  ya  madereva wa pikipiki mkoani Arusha hawana leseni za udereva na wengine hawajui sheria za barabarani
 
Hayo yamebainishwa na kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoani hapa Marson Mwakyoma wakati akifanya mahojiano na libeneke la kaskazini ofisini kwake
 
Alisema kuwa kutokana na ajali nyingi ambazo zimekuwa zikitokea kikosi cha usalama babarbarani kimefanya uchunguzi na kubaini kuwa zaidi ya madereva hao wamekuwa hawana leseni na  ambao wanayo wamekuwa hawajapata kwakufata sheria   na wengine hawajasoma kabisa.
 
Alisema kuwa ajali kutoka na ajali nyingi ambazo zimekuwa zikituokea mara mara wameamua kuanzisha operesheni maalumu  ya kusaka madereva ambao hawana leseni na wale ambao hawafati sheria za barabarani na iwapo wanawakamata basi watashika pikipiki zao na kuziweka ndani hadi pale dereva atakapokuja na  cheti kinachoonyesha amesoma .
 
Alibainisha kuwa mpaka sasa zaidi ya pikipiki 60 zimekamatwa  kutokana na makosa mbalimbali na madereva wake wamepelekwa katika chuo kimoja wapo cha udereva kupat aelimu na iwapo watamaliza basi watarudishiwa  pikipiki zao.
 
“ unajua madereva hawa wamekuwa wanalalamika kuwa garama ya kusoma ni kubwa hivyo tumeamua kuomba chuo kimoja cha udereva kupunguza bei na madereva hawa ambao watakuwa wamekamatwa wataenda pale kupata elimu hiii nadhani itasaidi kupunguza ajali nyingi ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara na kusabishia watu vilema vya maisha na wengine vifo”alisema Mwakyoma
 
Aidha alibainisha kuwa faini ya shilingi 30000 haisaidii kitu ila iwapo hawa madereva watafanya kozi hii basi anauhakika ajali za barabarani  zitapungua kabisa na mwishowe kwisha kabisa na alibainisha kuwa tangu operationi hiyo ianze ajali za pikipiki zimekuwa zikipungua siku adi siku huku akisema kuwa zoezi hili ni endelevu .
 
Aliwataka waendesha pikipiki hizi kwenda kusoma kwani wakijua sheria za barabarani itawasaidia hata ao wenyewe kutotoa rushwa ovyo kwani iwapo atajua sheria basi hamna askari yeyote atakaye mnyanyasa barabarani
 
Alitoa wito kwa madereva kwenda TRA kukata tin no kwani wasipokuwa na tin hawataweza kupata leseni zao huku akisisitiza kuwa tin hizo zinatolewa bure pasipo kuchajiwa kiasisi chochote cha fedha.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia