TANFOAM ARUSHA WALALAMIKIA KUHUJUMIWA
Magodoro 9 feki ya kampuni nyingine
yakiwa na nembo ya Tanfoam yakipakiwa na kampuni ya uwakala ya majembe
Action mart katika moja ya operesheri za kutambua bidhaa za tanfoam
zinazochakachuliwa na wafanyabishara
Meneja opereshen wa kampuni ya mejembe action mart,bw Mussa Matto alionyesha moja ya magodoro yanayouzwa na wafanyabiashara eneo la mbauda jijini Arusha,yasiyo ya kampuni ya Tanfoam likiwa limewekwa nembo ya Tanfoam
KAMPUNI ya kutengeneza magodoro ya Tanfoam mkoani Arusha imebaini kuhujumiwa kwa bidhaa zake na baadhi ya wafanyabiashara wajanja wasio waaminifu kwa kutumia nembo inayofanania katika magodoro ya kampuni nyingine na kuyauza kwa kutumia jina la kampuni hiyo.
Meneja opereshen wa kampuni ya mejembe action mart,bw Mussa Matto alionyesha moja ya magodoro yanayouzwa na wafanyabiashara eneo la mbauda jijini Arusha,yasiyo ya kampuni ya Tanfoam likiwa limewekwa nembo ya Tanfoam
KAMPUNI ya kutengeneza magodoro ya Tanfoam mkoani Arusha imebaini kuhujumiwa kwa bidhaa zake na baadhi ya wafanyabiashara wajanja wasio waaminifu kwa kutumia nembo inayofanania katika magodoro ya kampuni nyingine na kuyauza kwa kutumia jina la kampuni hiyo.
Akizungumza katika opareshion
inayoendeshwa na kampuni ya udalali ya Majembe Auction Mart ya jijiji
Arusha,kwa niaba ya Tanfoam ,Meneja Operesheni, Mussa Motto alisema kuwa ,zoezi
hilo linafanyika katika mikoa mbalimbali huku lengo likiwa ni kudhibiti wimbi
la uchakachuaji wa madogoro ya Tanfoam linalofanywa na baadhi wafanyabiashara.
Alisema kampuni hiyo ilibaini
kuwepo kwa magodoro feki ya Tanfoam na
kulazinika kuendesha operesheni ,ambapo hadi sasa zaidi ya magodoro 500 yamekwishakamatwa
yakiwa yamechakachuliwa na kuwekwa nembo ya Tanfoam
huku ubora wake ukionekana hafifu tofauti na magodoro halisi na kusababisha
malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa wateja wao.
Aliongeza
kuwa ,operesheni
hiyo imeanzia mkoani kilimanjaro na kufanikiwa kuwakamata baadhi ya
wafanyabiashara huku wengi wao wakifanikiwa kukimbia baada ya kuwepo
malalamiko ya wateja wao kulalamikia ubora hafifu
uliopo katika magodoro hayo ndipo
walipofikia hatua ya kuweka wakala kwa ajili ya kuthibiti hali hiyo.
Aidha alibainisha kuwa, kampuni
hiyo ya Tanfoam imelazimika kuendesha operation hiyo kwa kutumia kampuni ya
udalali ya Majembe ambayo imekuwa ikiyakamata na kuyaweka kwenye godauni lao na
baadaye kuteketezwa kwa moto.
Alifafanua kuwa
wafanyabiashara wamekuwa waitumia mbinu chafu ya kugonga nembo ya Tanfoam kwenye
magodoro ya kampuni nyingine na kuyauza kwa bei ile ile ,baada ya kufanikiwa
kutengeneza nembo ya muhuri wa moto unaofanania na ule wa Tanfoam.
Alisema ,hali hiyo ni
kinyume cha sheria na wamekuwa wakiwaibia wateja kwa kuwauzia bidhaa isiyo
haisi huku kampuni ikishindwa kufikia malengo ya mauzo ya bidhaa zake.
‘’Unajua katika biashara
yoyote kuna ushindani mkubwa sana wa kibiashara na kila mtu anabuni mbinu ya
kutumia ili kuweza kumudu soko la
ushindani, hivyo tumegundua kuwa asilimia kubwa sana ya wafanyabiashara
wamekuwa wakitumia nembo zetu kuuzia magodoro yao ‘’alisema Motto.
Aliongeza zaidi kuwa, operation
hiyo ni endelevu na itafanyika katika maeneo mbalimbali mkoani hapa ,na yeyote
atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na
kuchukuliwa bidhaa hizo feki.
Nao baadhi ya wakazi wa mbauda jijini Arusha walisema kuwa
zoezi la operesheni hiyo liwe endelevu na kutoa wito kwa kampuni ya Tanfoam kuhakikisha kuwa inadhibiti bidhaa
yake ili wajanja wasifanikiwa kuiga.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia