SEREKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR IKO KWENYE MCHAKATO WA KUAANDAA SHERIA

Seriklai ya mapinduzi ya Zanzibar imesema  iko katika mchakato wa kuandaa sheria itakayosimamia sera ya  mafuta visiwani humo.
Kauli hiyo imetolewa  na waziri wa waziri wa ardhi nyumba  maji na nishati Ramadhana Abdala Shaaban wakati akiwasilisha hotuba ya makadiro ya mapato na matumizi kwa wiraza yake kwa mwaka 2012-2013 katika baraza la wawakilishi .
Waziri huyo amesema tayari maandalizi ya sheria hiyo yamekamilika ambapo itasimamia zaidi masuala ya nishati visiwani humo.
Aidha amesema katika kuimarisha sekta ya nishati na madini serikali imewapeleka baadhi ya wataalamu nje ya nchi kwaajili ya mafunzo ikiwemo suala la mafuta na gesi.
Hatua hiyo inakuja wakati ambapo seriklai ya mapinduzi ya zanziba inasubiri kuondolewa kwa   mafuta na gesi asilia katika masuala ya Muungano .

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia