MSAJILI WA ICTR ATEULIWA MSHAURI MAALUM WA MASUALA YA KUZUIA MAUAJI YA KIMBARI

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon amemteua Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), Adama Dieng, raia wa Senegal, kuwa Mshauri Maalum wa masuala ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari.
Taarifa iliyotolewa Jumanne na Idara ya Mawasiliano kwa Umma, ilisema, Dieng ambaye amekuwa akitumikia nafasi yake ya sasa ICTR tangu mwaka 2001, anachukua nafasi ya Frances Deng, ambaye  Katibu Mkuu huyo anamshukuru kwa utumishi wake uliotukuka. Deng ambaye ni raia wa Sudan alikuwa anatumikia katika nafasi hiyo tangu Mei 2007.
‘’Akiwa mtaalam wa sheria na masuala ya haki za binadamu, Dieng ana utumishi uliotukuka na mchango wa pekee katika kuimarisha utawala wa sheria, mapambano dhidi ya kushitaki wahalifu na kujenga uwezo katika nyanja za mahakama na taasisi za kidemokrasia ikiwa ni pamoja na utafiti, machapisho na vyombo vya vya habari,’’ taarifa imesema.
‘’Alichangia pia uanzishwaji wa mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali barani Afrika,’’ taarifa ilifafanua. Dieng alianza kazi kama Msajili wa Mahakama ya Kanda na Kazi nchini Senegal na kutumikia pia nafasi ya Msajili wa Mahakama Kuu ya Senegal kwa miaka sita.
Baadaye Dieng alijiunga na mashirika mbalimbali ya kimataifa akitumikia nafasi mbalimbali.Alizaliwa Mei 22, 1950 na ni mhitimu wa shahda ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dakar.Ametunukiwa vyeti mbalimbali kikiwemo cha Kituo cha Utafiti katika Chuo cha Sheria za Kimataifa, kilichopo The Hague, Uholanzi.
Ofisi ya Mshauri Maalum wa Kuzuia Mauaji ya Kimbari, ilianzishwa mwaka 2004.Imepewa kazi na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ya kukusanya na kutathmini taarifa kuhusu hali ambayo inaweza kusababisha mauaji ya kimbari kutokea.
Ofisi hiyo pia ina jukumu la kumshauri katibu Mkuu wa UN, na kupitia kwake, Baraza la Usalama, kutoa mapendekezo ya kuzuia mauaji ya kimbari.Ofisi hiyo pia hufanya mawasiliano na mfumo wa UN wa hatua za kuchukua ili kuzuia mauaji ya kimbari au uhalifu unaohusiana nao.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia