Serikali wilayani hai imesambaza katiba zaidi ya 200 vijijini

Serikali wilayani  Hai  Mkoani Kimanjaro imefanikiwa kusambaza katiba zaidi ya 200 katika vijiji mbalimbali, tarafa, kata, taasisi pamoja na vyama vya siasa wilayani humo

Lengo la hatua hii ni kuwawezesha wananchi wa wilaya ya Hai kuweza kushiriki kikamilifu katika mjadala wa marekebisho  ya katiba mara tume  ya kukusanya maoni itakapokuwa wilayani Hai

Mkuu wa Wilaya ya Hai Bwana Novatus Makunga amesema hayo katika mahojiao na mwandishi wa habari hizi  juu ya makakati wa Serikali katika Wilaya hiyo katika kufanikisha mjadala wa Maoni ya Katiba

Bwana Maunga  amesema  Ofisi yake imepeleka  katia idara za Serikali nakala  16 za Katiba  , Ofisi za Tarafa  katiba  tatu, na Ofisi za Kata  katiba 14

Mkuu huyo wa Wilaya amefafanua kuwa nakala 120  za Katiba  zimepelekwa katika Ofisi za Vijiji, nakala 41 zimepelekwa katika madhehebu ya dini, mashirika yasiyo ya Kiserikali yamepatiwa nakala sita

Aidha Vyama vya Siasa  vimepatiwa  nakala saba za katiba ili wananchama wao waweze kuipitia  na kuijadili kabla ya kutoa maoni mbele ya Tume ya kukusanya maoni itakapokuwa katika Wilaya hiyo. Amesisitiza Bwana Makunga leo

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia