WALIOACHIWA HURU WATAKA ICTR IWASIKILIZE KUPATA NCHI YA KWENDA KUISHI

Watu wanne kati ya watano walioachiwa huru na Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) wamemwomba Rais wa Mahakama hiyo kuunda jopo litakalosikiliza madai yao kuhusu kukosekana kwa nchi ya kuwapokea.
Watu hao ni pamoja na mawaziri watatu wa zamani wa Rwanda, Andre Ntagerura(Usafirishaji), Jerome Bicamumpaka (Mambo ya Nje) na Casimir Bizimungu (Afya) pamoja na Brigadia Jenerali Gratien Kabiligi. Wote wanaendelea kuishi mjini, Arusha, Tanzania,makao makuu ya ICTR katika nyumba maalum chini ya uangalizi wa mahakama hiyo.
Katika maombi yaliyotiwa saini na Wakili Philippe Larochelle kutoka Canada, walalamikaji hao wanataka majaji watoe maombi kwa nchi mbalimbali kushirikiana ili kuhakikisha kwamba wanapatiwa nchi za kuwapokea kwenda kuishi kama watu wengine.
Kwa mujibu wa maombi hayo, Ntagerula anataka kwenda kuishi Canada, Ufaranza au Uholanzi wakati Kabiligi anapenda kwenda Ufaransa. Kwa upande wao Bizimungu na Bicamumpaka wanataka kwenda nchini Canada.
Wakirejea kwenye vifungu vya sheria za ICTR, walalamikaji hao wamekiri kwamba suala la kutafutiwa nchi za kuishi kwa wanaoachiwa huru na ICTR halikutajwa kama mojawapo linalozitaka linazozitaka nchi kutoa ushirikiano pasipo ucheleweshwaji usio wa lazima.
Lakini wanadai kwamba njia thabiti ya kurekebisha hali hiyo ambayo inakiuka haki zao za msingi baada ya kuachiwa huru ni kwa mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa kutumia mamlaka yake ya kisheria kuziomba moja kwa moja nchi wanamchama wa UN kutoa ushrikiano unaohitajika ili zipatikane nchi za kuwapokea walalamikaji.
‘’Kuungwa mkono kwa pendekezo kwamba kupatiwa nchi za kuwapokea ni sahihi unaweza kupatikana katika maombi lukuki yaliyotolewa na viongozi waandamizi wote wawili wa mahakama hiyo, Msajili na Rais wake kwenda Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakiomba wasaidiwe kutatua tatitizo la kutopatikana kwa nchi za kuwapokea walioachiwa huru,’’ wanadai katika sehemu ya maombi yao.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia