MENEJA WA TRA ARUSHA HATARINI KUPELEKWA MAHAKAMANI

MENEJA  wa TRA mkoani  Arusha ,Evaristi Kileva yupo hatiani kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kosa la kudharau na kukaidi  amri halali ya mahakama iliyotolewa hivi karibuni ya kutaka akabidhi magari saba ya mshtakiwa Mwale baada ya mahakama kubaini kwamba hakuna sababu za msingi za kuendelea kuyashikilia.

Mmoja wa wanandugu wa wakili Mwale (jina limehifadhiwa ) alisema kuwa baada ya hukumu kutolewa, mahakama ilitoa order ya kumtaka meneja wa TRA mkoani Arusha kukabidhi mara moja magari hayo.

Tangu kutolewa kwa hukumu hiyo, machi 6 mwaka huu meneja huyo amekuwa akipiga danadana kwa kushirikiana na mawakili wa serikali hatua ambayo inadaiwa huenda ana maslahi binafsi na magari hayo.

Alisema alipofika katika ofisi za TRA mkoni Arusha na kuonana na Meneja huyo na kumkabidhi hati ya hukumu pamoja na oda ya mahakama ,chakushangaza meneja huyo  aliendelea kuwasumbua huku akidai anasubiri majibu kutoka kwa bosi wake makao makuu.

Aliongeza kuwa kwa sasa wapo mbioni kuiomba mahakama itoe hati ya  kumtia mbaroni  meneja huyo na kumfungulia mashtaka kwa kosa la kuvunja sheria za nchi kwa kukaidi amri halali ya mahakama ambayo imekwisha tolewa .

Awali hakimu wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha,Charles Magesa alitoa hukumu kuwa , wakili Mwale akabidhiwe magari yake baada ya upande wa serikali kushindwa kuthibitisha uhalali wa kuyashikilia baada ya kudai kuwa ni matunda ya uhalifu wa kupatikana na fedha chafu.

Mshitakiwa Mwale ambaye kwa sasa bado anashikiliwa mahabusu katika gereza kuu la kisongo jijini hapa,aliamua kuwasilisha hoja ya kupinga kukamatwa kwa magari hayo, ambapo kesi hiyo iliunguruma kwa muda huku upande wa serikali ukiwakilishwa na mawakili ,Fredrick Manyanda na Neema Ringo .

Ambapo  mawakili wa serikai waliiambia mahakama hiyo kuwa, magari hayo yanashikiliwa na mamlaka ya mapato TRA  kwa sababu yalikuwa hayajalipiwa ushuru wakati yakiingizwa nchini,kitendo ambacho TRA imekuwa ikikanusha  mahakamani hapo na kudai kuwa wao hawadai ushuru wa magari hayo.

Hakimu Mageza baada ya kupitia hoja za pande zote mbili alitoa hukumu ya kutaka magari hayo yarejeshwe kwa Mwale ili kupisha kesi ya msingi iweze kuendelea.

Hata hivyo hukumu hiyo haikuwaridhisha upande wa serikali na kuamua kukata rufaa mahakama kuu ambapo jaji wa mahakama hivyo Kakusulo Sambu alipitia hoja za pande zote mbili,kabla ya kutupitia mbali maombi ya upande wa mashtaka  na kubariki hukumu ya  hakimu Magesa ya kutaka  magari hayo yarejeshwe kwa Wakili Mwale, kitendo ambacho hadi sasa kimeshindwa kutekelezwa.

Kwa upande wa Meneja wa TRA Arusha,Evalist Kileva alipohojiwa kuhusiana na kukaidia amri ya mahakama alisema kuwa kwa sasa hawezi kulizungumzia suala hilo ila anasubiri maelekezo kutoka ngazi za juu,bila kufafanua ni ngazi zipi.

Hata hivyo wanasheria mbalimbali waiwemo wadau wa sheria hapa nchini wamedai kuwa kitendo cha meneja wa TRA mkoni Arusha,kukaidi amiri ya mahakama ni kinyume cha sheria na anatakiwa akamatwe na kufunguliwa mashtaka ya kiidharau mahakama.

habari na mdau wa libeneke la kaskazini Josephy Ngilisho

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia