MKUU WA WILAYA YA HAI APIGA MARUFUKU KILIMO CHA MTONI

mkuu wa wilaya ya hai bw novatus makunga ametoa mwezi mmoja wa kuondolewa kwa shamba ya miwa katika chanzo cha mto ngarewarikoi katika kijiji cha mboreni na pia kuchuliwa hatua za kisheria kwa wamilikiwa wa mifereji wanaopuuzia ratiba ya kurejesha maji ya mto.

Ameeleza kuwa hatua hizo zinachukuliwa  ili kuokoa maisha ya wananchi wa maeneo ya vijiji vya tambarare ambao wapo katika hali mbaya kutokana na hali ya ukame.

mkuu huyo wa wilaya amefikia hatua hiyo katika kikao alichohitisha cha pamoja kati ya kamati zinazosimamia matumizi ya maji ya mto huo,viongozi wa vijiji na  wataalamu kutoka mamlaka ya bonde la mto pangani.

Kikao hicho ambacho pia kilihudhuriwa na madiwani katika kata za mto huo alikihitisha kwa lengo la kujadili taarifa ya kamati aliyoiunda kufuatilia shughuli za kibinadamu zinazofanyika katika bonde la mto huo ambazo zinadaiwa kuchangia upatikanaji wa maji katika maeneo hayo.

Makunga alisema kuwa pande zote za watuamiaji wa maji katika mto huo mwamekubaliana kuondolewa kwa shamba hilo la miwa lililopo katika chemuchemu kijiji cha mboreni ndani ya mwezi mmoja.

Amesema baadhi ya ukiukaji wa matumizi ni pamoja na mifereji ya kijiji cha lemira na nure yam to wawu kutorudisha maji mtoni tangu ilipojengwa na uharibifu wa korongo la mto kufukiwa na mkulima mmoja.

Kadhalika amefafanua kamati kugundua chemchem ya kijiji cha mbweera inatakiwa kuoteshwa miti ya kutuna maji na siyo aina ya mijohoro kwani miti hiyo inakausha maji pamoja na hatua za kuzuia mifugo kuvamia mto.

Ameeleza kuwa hatua za haraka ziizofikiwa na kikao hicho ni pamoja na kuhakikisha vijiji vyote vilivyopo maeneo ya milimani vyenye mifereji kutoka katika mto huo vinarudisha maji kila ifikapo saa kumi jioni na kuyaancha mpaka asubuhi ya siku inayofuata

Makunga alisema kuwa kupitia sheria za mamlaka ya bonde la pangani ambazo ndiyo zinasimamia matumizi na maendeleo ya mito ya maeneo hayo,watakaobainika watatozwa faini ya shilingi laki tano

Aidha amesema kuwa watumiaji hao walikubaliana mifereji yote ikarabatiwe ili isipoteze maji na pia kuweka milango ya kudhibiti kiasi cha maji na miti ya asili kupandwa kandokando ya mto na mifereji.

Ameeleza pia wamekubaliana kusitishwa kwa shughuli za kilimo katika bwawa la magadini ifikapo mwishoni mwa wezi huu ili liweze kufukuliwa kwa ajili ya kukusanyia maji na kuyahifadhi


Mmoja ya mwananchi wa jamii ya wafugaji julius joshua ameeleza kuwa matatizo ya mto huo yametokana na wataalamu wa kilimo na mifugo kushindwa kuwajibika ipasavyo

Ameeleza kuwa wengi wamekuwa wakikaa zaidi ofisini bila kufuatilia mto huo ambao uliwahi kuimarishwa kwa ajili ya kukuza kilimo cha mbogamboga na pia matumizi ya wafugaji

Naye mwenyekiti wa kamati  ya wananchi hao ya ufuatiliaji wa korongo la mto huo shaban mahmoudy ameeleza kuwa pendekezo la kufukuliwa kufukuliwa kwa bwawa la magadini wataliingiza katika mikutano ya vijiji husika ili liweze kupata Baraka za wananchi wote

Vijiji vinavotegemea maji yam to huo ni pamoja na msikitini,kambi ya mkaa,lerai,magadini na kingereka

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia