ICTR YAKATAA MAOMBI YA JOPO LA KUSIKILIZA KILIO CHA WALIOACHIWA HURU
Rais
wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) Jumanne
alikataa maombi ya watu wanne walioachiwa huru kutaka aunde jopo
litakalosikiliza madai yao kuhusu kukosekana kwa nchi za kuwapokea
kwenda kuishi.
Rais
huyo Jaji, Vagn Joensen amesema amezingatia uamuzi uliotolewa na
Mahakama ya Rufaa ya mahakama hiyo, Novemba 2008 katika kesi ya Waziri
wa zamani wa Usafirishaji wa Rwanda, Andre Ntagerura uliotolewa miaka
miwili baada ya kuachiwa kwake huru.
‘’Nimelazimika
kufuata tafsiri ya sheria kama ilivyotolewa na Mahakama ya Rufaa,’’
alisema Rais huyo wa ICTR.’’ Sheria husika haitoi mamlaka yoyote kwa
Mahakama kuyakubali maombi ya walalamikaji. Hivyo sina sababu ya kuunda
jopo la kusikiliza maombi hayo,’’ alisema.
Waliowasilisha
maombi hayo ni pamoja na mawaziri watatu wa zamani wa Rwanda, Andre
Ntagerura(Usafirishaji), Jerome Bicamumpaka (Mambo ya Nje) na Casimir
Bizimungu (Afya) pamoja na Brigadia Jenerali Gratien Kabiligi. Wote
wanaendelea kuishi mjini, Arusha, Tanzania,makao makuu ya ICTR katika
nyumba maalum chini ya uangalizi wa mahakama hiyo.
Katika
maombi yaliyotiwa saini na Wakili Philippe Larochelle kutoka Canada,
walalamikaji hao wanataka majaji watoe maombi kwa nchi mbalimbali
kushirikiana ili kuhakikisha kwamba wanapatiwa nchi za kuwapokea kwenda
kuishi kama watu wengine.
Kwa
mujibu wa maombi hayo, Ntagerula anataka kwenda kuishi Canada, Ufaranza
au Uholanzi wakati Kabiligi anapenda kwenda Ufaransa. Kwa upande wao
Bizimungu na Bicamumpaka wanataka kwenda nchini Canada.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia