LUBANGA JELA MIAKA 14, MAHAKAMA UFARANSA YAZUIA MNYARWANDA KUREJESHWA KWAO

Wakati Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai, wiki hii imemhukumu kifungo cha miaka 14 jela kiongozi wa waasi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Thomas Lubanga, kwa uhalifu wa kivita, Mahakama ya juu nchini Ufaransa imebatilisha uamuzi wa kumrejesha raia wa Rwanda kwao ili akashitakiwe kwa makosa ya mauaji ya kimbari. 

ICC
Lubanga apata miaka 14 jela: Majaji wa mahakama hiyo Jumanne wiki hii walimhukumu kifungo cha miaka 14 jela kiongozi wa waasi katika DRC, Thomas Lubanga, kwa uhalifu wa kivita. Hukumu hiyo imepokelewa vema, huku serikali ya DRC ikisema ni ishara chanya kwa amani ya baadaye katika jimbo lenye migogoro la Kivu. Wakati muungano wa Mahakama ya Kimaifa ya Makosa ya Jinai ukielezea uamuzi huo kama tukio muhimu katika kupambana na uonevu katika jimbo hilo, upande wa mashitaka umesema umepeleka ujumbe ulio wazi kwamba wahusika wa makosa hayo hawataachwa bila kuadhibiwa. 
Wakili wa waasi wa Darfur aomba msaada UN: Jumatano wiki hii wakili wa Abdallah Banda na Mohammed Jerbo aliliomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuichulia hatua serikali ya Sudan kwa madai ya kuzuia haki isitendeke kwenye kesi ya wateja wake. Karim Khan alielezea kuwa upande wa utetezi hauwezi kufanya uchunguzi wa maaana kwa sababu Sudan imekataa kushirikiana na mahakama. Washitakiwa wote wanatuhumiwa kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu kufuatia shambulizi la 2007 katika ngome ya kijeshi ya Haskanita, ambapo walinda amani wa kimataifa 12 waliuawa.
Kesi ya Wakenya wanne kuanza Aprili 2013: Mahakama Jumatatu wiki hii ilipanga Aprili 10 na 11, 2013, kama tarehe za kuanza kwa kesi mbili za Wakenya wanne, ambao ni Naibu Waziri Mkuu Uhuru Kenyatta, Mbunge William Ruto, aliyekuwa Mkuu wa Utumishi, Francis Muthaura na Mwandishi Joshua arap Sang. Wanatuhumiwa kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu kufuatia vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi mkuu wa rais mwaka 2007. 
UFARANSA
Mahakama yazuia raia wa Rwanda kurejeshwa kwao: Mahakama ya Juu nchini Ufaransa imebatilisha maamuzi ya awali yaliyotolewa Machi 29, na Mahakama yaRouen kwamba Claude Muhayimana anapaswa kurejeshwaRwanda kukabiliana na makosa ya mauaji ya kimbari.Rwanda inamhitaji Muhayimana kwa makosa yaliyotendeka katika mkoa wa Kibuye mwaka 1994.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia