NMB YASAIDIA WANAFUNZI SAME



Meneja wa huduma kwa wateja wa benki ya NMB tawi la Same , Anna Efrem (kushoto) akikabidhi zawadi kwa mwanafunzi Omari Silayo baada ya kuibuka mshindi wa kwanza kwa wanafunzi wa shule ya msingi Majengo iliyopo wilayani Same,kujibu maswali vizuri juu ya ufahamu wa masuala ya kibenki kuhusu mpango wa NMB  Financial Fitness uliozinduliwa na benki hiyo kwa watoto wilayani humo.

Benki ya NMB wilayani Same imefanikiwa kwa kiwango kikubwa kutoa elimu ya mpango wa uelewa wa masuala ya fedha(Financial Fitness) kwa watoto wa shule za msingi uliozinduliwa hivi karibuni ambao umewajengea uwezo watoto kuhifadhi fedha mahali salama tangu wakiwa na umri mdogo.

Meneja wa huduma kwa wateja wa NMB tawi la Same , Anne Efrem alibainisha hayo wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya  mpango huo uliofanyika katika shule ya msingi majengo  na kuwashirikisha  wanafunzi mbalimbali wa shule za msingi kutoka wilayani humo.

Alisema mpango huo utasaidia watoto  kuwa na tabia ya kuhifadhi fedha benki wakiwa na umri mdogo bila kuwa na matumizi mabaya ,hali ambayo itasaidia kupunguza upotevu ovyo wa fedha na kuwataka watoto hao kuitoa pia elimu hiyo kwa wazazi wao.

Efrem alifafanua kuwa  mkakati wa benki ya NMB ni kuufikisha mpango huo kwa jamii nzima wakianzia na watoto na baadae kuufanya kila mmoja kuwa na uelewa wa masuala ya kibenki katika  kutumia fedha kwa uangalifu.


Aidha alisema benki ya NMB kupitia sera  yake ya msaada kwa jamii ambayo ipo kwa ajili ya mambo matatu,Afya,Elimu na Michezo imeanzisha mpango huo unaofanyika nchi nzima kwa kujikita zaidi kutoa elimu hiyo kwa watoto waliopo kwenye shule za msingi hapa nchini.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia