16 BORA COPA COCA-COLA KUANZA J’MOSI
16
bora ya michuano ya Copa Coca-Cola 2012 inaanza kesho (Julai 7 mwaka
huu) kwa mechi nne zitakazokutanisha timu nane kati ya 16 zilizofuzu
hatua hiyo. Mechi hizo za 16 bora zitachezwa kwenye viwanja vya
Kumbukumbu ya Karume na Tanganyika Packers vya Dar es Salaam.
Ruvuma
iliyoongoza kundi A itacheza na Temeke iliyoshika nafasi ya tatu kundi
C. Mechi hiyo itaanza saa 2.30 asubuhi Uwanja wa Karume. Mechi nyingine
ya asubuhi itakayochezwa Tanganyika Packers itawakutanisha washindi wa
pili kundi A Kigoma dhidi ya Mara walioshika nafasi ya nne kundi C.
Mechi
za jioni kwa kesho zitakazoanza saa 10 kamili jioni zitakuwa kati ya
Mjini Magharibi na Kagera kwenye Uwanja wa Karume wakati Morogoro na
Pwani zitaumana kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers ulioko Kawe, Dar es
Salaam.
Hatua
ya 16 bora itakamilika keshokutwa (Julai 8 mwaka huu) kwa mechi za
asubuhi kati ya Kinondoni na Rukwa kwenye Uwanja wa Karume, na Dodoma
dhidi ya Arusha kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers. Mechi za jioni siku
hiyo ni kati ya Kilimanjaro na Mwanza (Uwanja wa Karume) na Tabora na
Tanga (Tanganyika Packers).
Timu
zitakazoshinda zitaingia hatua ya robo fainali itakayochezwa Julai 10
na 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Nusu fainali
itachezwa Julai 13 mwaka huu, na kufuatiwa na mechi ya mshindi wa watatu
na fainali ambazo zote zitachezwa Julai 15 mwaka huu.
SABA WAPATA ITC KUCHEZA KENYA, MSUMBIJI
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa
(ITC) kwa Watanzania saba kucheza mpira wa miguu katika nchi za Kenya na
Msumbiji.
TFF
imetoa hati hizo kwa wachezaji hao baada ya kuombewa na Shirikisho la
Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu la
Msumbiji (FMF) ili waweze kucheza katika klabu za nchi hizo.
Wachezaji
waliokwenda Bandari ya Kenya na klabu walizokuwa wakichezea nchini
kwenye mabano ni David Naftali (huru), Meshack Abel (huru), Mohamed
Banka (huru) na Thomas Mourice (Mtibwa Sugar).
Klabu
ya CD Madchegde ya Msumbiji imewachukua wachezaji Hassan Hassan
Mustapha kutoka Mgambo Shooting ya Tanga, na Abdallah Ally Abdallah na
Thobias David Silas kutoka klabu ya daraja la kwanza ya Transit Camp ya
Dar es Salaam.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia