ADAI MWENDESHA MASHITAKA KAJICHANGANYA USHAHIDI KESI YA NGIRABATWARE

Timu ya utetezi katika kesi inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Mipango wa Rwanda, Augustin Ngirabatware, Jumanne iliiomba Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) kuzikataa hoja za mwendesha mashitaka anazodai kumwunganisha mteja wake na mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.
 
‘’Mwendesha mashitaka amevurunda ushahidi wake mwenyewe kwa kutoa madai ambayo hayaungwi mkono na ushahidi wowote,’’ alisema Wakili Kiongozi, Mylene Dimitri mbele ya Mahakama iliyokuwa inaongozwa na Jaji, William Sekule.
 
Wakili huyo alikuwa anatoa hoja za mwisho kupitia mtandano wa video kutoka nchini Canada. Alidai kwamba baadhi ya mashahidi wa mwendesha mashitaka nao walikuwa watuhumiwa hali ambayo iliwafanya watoe ushahidi kupata upendeleo fulani.
 
Kwa mujibu wa wakili huyo, mashahidi wa aina hiyo walidanganya na kutunga ushahidi dhidi ya mteja wake ili wapate adhabu ndogo au kuachiwa toka gerezani.
 
Aliulaumu pia upande wa mwendesha mashitaka kwa kudai kuwa Ngirabatware alihusika na uhalifu uliofanywa na wanamgambo wa Interahamwe. Alifafanua kwamba mteja wake hakushitakiwa kwa makosa ya kuwa na mamlaka juu ya Interahamwe.
 
 
Waziri huyo wa zamani anashitakiwa kwa kula njama za kufanya mauaji ya kimbari, mauaji ya kimbari au kushiriki mauaji hayo, uchochezi, kuteketeza kizazi na ubakaji kama uhalifu dhidi ya binadamu.
 
Uwasilishaji wa hoja za mwisho unaendelea Jumatano.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia