MTENDAJI ATUHUMIWA KUNYANYASA FAMILIA

MTENDAJI wa kata ya  Usa river wilayani Arumeru, John Laizer   anatuhumiwa kuinyanyasa  familia moja na kuisababisha kuishi kwenye mazingira magumu ya hofu ambayo yanatishia usalama na uhai wao na kuzuia uendelezaji wa nyumba inayojengwa kwa ajili ya familia hiyo ya mama na watoto wake wawili.

Kwa mujibu wa mmoja wa familia hiyo,Ephata Abrahamu Swai, mkazi wa kijiji cha Emanyata, amewaambia wanahabari kijijini hapo kwamba Mtendaji huyo amekuwa akitumia madaraka yake vibaya kwa kutaka aabudiwe kama mungu  mtu kuzuia  familia hiyo isiweze kuendeleza nyumba inayojengwa na ndugu zake na mwanamke  kwa ajili ya familia hiyo bila ridhaa yake.

Ephata, amemtuhumu kaka mkubwa wa familia hiyo ya Swai,aitwae Simion Abraham Swai,  ambae pia ni ni mzee wa Kanisa la AMEC, kwa kushirikiana na mtendaji huyo kuchochea mgogoro , kwa kuwa alitaka  kuuza eneo la mdogo wake aitwae Joseph Abraham Swai, analoishi na  mkewe ,ambae kwa sasa yuko mahabusu akikabiliwa na tuhuma za kesi ya mauaji .

Ephata ,amesema kabla ya mdogo wao kupatwa na mkasa wa kutiwa mbaroni alikuwa akiishi na mke wake aitwae Anande (40) ambae wamezaa nae watoto wawili mmoja wa kiume aitwae Emanuel na mwingine wa kike aiwae Jesca.

Alisema kuwa katika mgogoro huo ndugu wote sita wa familia hiyo na ndugu wa koo wapatao 30 ,walikaa katika kikao kilichofanyika Juni 20 mwaka huu na kukataa kuuzwa kwa eneo hilo ,na badala yake walikubaliana ndugu zake mwanamke waendelee na ujenzi wa nyumba hiyo lakini ilipofika Juni 10 walipokea amri toka kwa Mtendaji wa Kata hiyo akizuia ujenzi huo bila ufafanuzi zaidi.

Ephata,amesema walifikisha swala hilo ofisini kwa mtendaji wa Kata na pamoja na maamuzi  ya kikao cha ukoo ambayo yaliruhusu ujenzi kuendelea na mtendaji huyo aliyaafiki na  baada ya muda wa wiki moja mtendaji kupitia kwa Mwenyekiti wa Kitongoji aitwae Jeremia Abel Urio, walipokea amri ya kuzuia tena ujenzio usiendelee bila ufafanuzi .

Wameshangazwa kuona mtendaji anakuwa ni kikwazo na kutokana na maagizo  yake anayoyatoa kupitia njia ya simu ya mkononi,kwa mwenyekiti wa Kitongoji, kuzuia eneo hilo lisiendelezwe kitendo ambacho ni matumizi mabaya ya madaraka yake kwa kuwa anasababisha migogoro katika familia na jamii .

Mtendaji huyo, alipotakiwa kutoa ufafanuzi  juu ya sakata hilo alidai kuwa yeye alitumia mamlaka ya kuzuia ujenzi huo ili kupata mwafaka wa wanafamilia hao,hata hivyo alishindwa kufafanua iwapo amefanikiwa kumalizika kwa mgogoro .

Ephata amesema tayari kilio chao hicho wameshakifikisha kwaMkuu wa wilaya ya Arumeru, Deus Mnasa Sabhi, kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi wa mgogoro huo ili kuwezesha familia hiyo kundeleza eneo lao,hata hivyo mkuu huyo ameahidi kushughulikia suala hilo.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia