TAASISI YA KURITHI KAZI ZA ICTR YAZINDULIWA RASMI

Rais wa Taasisi ya Kimataifa itakayorithi kazi za Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (MICT),Jaji Theodor Meron Jumatatu ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuongeza juhudi za pamoja katika kuwasaka na kuwatia mbaroni watuhumiwa wa mahakama hiyo ambao bado hawajakamatwa akiwemo Felicien Kabuga anayesadikiwa kuwa kinara wa mauaji hayo.
“Taasisi hii haina budi na itafanyakazi na nchi mbalimbali duniani kuhakikisha kwamba washitakiwa hao wa ICTR wanaletwa mbele ya haki. Hatuwezi kuwaachia washitakiwa hao wa makosa mazito kabisa kuwa nje ya mkondo wa sheria,’’ alisisitiza Rais wa MICT,Jaji Theodor Meron, wakati wa sherehe ya uzinduzi wa chombo hicho.
‘’Kama Rais wa Taasisi hii, naahadi kufanya kila ninaloweza kwa kushirikiana na mwendesha Mashitaka (Hassan Bubacar) Jallow kuhakisha kwamba nchi zinashirikiana nasi kuwakamata na kuwashitaki watuhumiwa waliobaki,’’ alisema.
Taasisi hiyo ya MICT inachukua kazi muhimu zitakazokuwa zimebakia kukamilishwa na ICTR na Mahakama nyingine ya Kimataifa ya Uhalifu ya Kivita katika Yogoslavia ya zamani (ICTY).
Washitakiwa wengine wawili ambao pia wamepangwa kushughulikiwa na MICT ni pamoja na Waziri wa zamani wa Ulinzi, Augustin Bizimana na Kamanda wa zamani wa kikosi cha Walinzi wa Rais, Protais Mpiranya.
Kiongozi huyo wa MICT pia alisema kwamba atatekeleza kazi nyingine zilizopewa taasisi yake ikiwa ni pamoja na ulinzi wa waliathiriwa na uhalifu huo pamoja na mashahidi,uhifadhi wa nyaraka na kumbukumbu na kusimamia utekelezaji wa adhabu kwa waliotiwa hatiani.
Kwa mujibu wa Jaji Meron MICT itashughulikia pia maombi ya wafungwa watakaoomba kuachiwa huru mapema kwa msamaha.
Jaji huyo alitumia nafasi hiyo pia kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzaniakwa kuipatia eneo la kujenga ofisi za MICT mjini, Arusha, ambako nyaraka na kumbukumbu za ICTR zitahifadhiwa.
Akizungumza katika sherehe za uzinduzi huo, Mwendesha Mashitaka wa MICT, Hassan Bubacar Jallow, alisema, watuhumiwa wengine sita waliobakia na kesi zao kuhamishwa kwenda kusikilizwa nchini Rwanda hawatasemahewa kwani nao wataendeelea kusakwa vikali, kwani kinyume chake itakuwa ni sawa na kushindwa kwa mfumo wa utendaji haki wa kimataifa.
‘’Juhudi za mfumo wa haki wa kimataifa utakuwa unaathiriwa vibayakamaviongozi hao wa mauaji ya kimbari hawatakamatwa na kuwajibishwa kwa vitendo vyao,’’ alisisitiza.
Washitakiwa hao sita ni pamoja na luteni kanali mmoja, mameya watatu, inspekta wa zamani wa polisi na mmiliki wa mgahawa mmoja.
Sherehe ya uzinduzi wa MICT imehudhuriwa na viongozi mbalimbali mashuhuri wakiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Kitengo cha Sheria, Stephen Mathias, Waziri wa Sheria na Katiba wa Tanzania, Mathias Chikawe, Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Rwanda, Martin Ngoga, Rais wa ICTR, Jaji Vagn Joensen pamoja na majaji wengine wa ICTR na wafanyakazi. 

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia