Ticker

6/recent/ticker-posts


Marafiki wa aliyekuwa mshiriki wa Miss Tanzania 2013 akitokea Miss Ilala, Martha Gewe wakiwa na huzuni.KWELI kifo hakina huruma jamani! Mshiriki wa Miss Tanzania 2013 akitokea Miss Ilala, Martha Gewe, mkazi wa Tabata Segerea, Dar amefariki dunia baada ya kuugua ghafla, Ijumaa Wikienda linakupa zaidi.
Martha amekutwa na mauti katika Hospitali ya Mkoa wa Ilala, Amana jijini Dar es Salaam, Ijumaa iliyopita ambako alikimbizwa baada ya kuugua na madaktari walibaini kwamba, malaria ilipanda kichwani.  Marehemu Martha Gewe enzi za uhai wake. Watimanywa usiku wa kuamkia leo, kule jijini London, Uingereza alifurukuta kugombea Taji la Miss World! Habari zaidi zinasema kuwa mrembo huyo hakuwa akisumbuliwa na ugonjwa wowote huko nyuma na alionekana mwenye afya njema huku mipango yake ikiwa imelenga jinsi atakavyoisherehekea Sikukuu ya Krismasi. “Lakini Jumatano iliyopita alianza kuumwa, alisema anahisi homa ambayo baadaye ikabainika ni malaria. 

Post a Comment

0 Comments