WAREMBO 17 KUCHUANA REDS MISS NORTHERN ZONE

Baadhi ya ‘Wazee wa Ngwasuma’ wakiwa jukwaani.
Rais wa bendi hiyo, Nyoshi El- Saadat (wa pili kushoto), akiongoza safu ya waimbaji na mnenguaji machachari, Suzan Chubwa (Queen Suzi, katikati).
Wanenguaji wote wa bendi hiyo wakiwa kwenye pozi la pamoja.
Mpiga tumba akipagawisha.
Mpiga ‘drums’ wa bendi hiyo akiwajibika.
Rapa Toto Kalala akiwa katika majukumu yake.
Baadhi ya wanenguaji wa kike wa bendi hiyo wakiwa katika pozi.


Nyoshi El-Saadat (kushoto), akibadilishana mawazo na baadhi ya wanenguaji wake.
Jumla ya warembo 17 wanaoshiriki shindano la Reds Miss Northern Zone wanataraji kuchuana vikali mnamo julai 5 mwaka huu kwa lengo la kumpata mrembo atakayeiwakilisha kanda hiyo katika shidano la Miss Tanzania.

Warembo hao wanataraji kuingia kambini juni 28 mwaka huu katika ukumbi wa Triple A ambapo watakuwa chini ya walimu Zakhia Ramadhan ,Angel Justaz na Joseph Mgani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa kampuni ya Mwandago Investment Entertainment,Faustine Mwandago ambaye ndiyo mwandaaji wa shindano hilo alisema kuwa warembo kutoka jijini Tanga tayari wameshatinga Arusha .

Alisema kuwa katika shindano hilo warembo kutoka mkoani Manyara wako watano,Kilimanjaro wako 4,Tanga wanawakilishwa na warembo 3 na mwenyeji Arusha inawakilishwa na warembo 5.

Mwandago,alisisitiza ya kwamba mwaka huu shindano hilo litanogeshwa na bendi ya F M Academia kutoka jijini Dar es salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni mbunge wa viti maalumu mkoani Arusha,Catherine Magige(CCM).

Hatahivyo,alisema kwamba mwaka huu wamejipanga katika suala la hali ya hewa ambapo kutakuwa na majiko ya moto ya kisasa kwa ajili ya kukabiliana na hali ya hewa ya baridi ukumbini huku upande wa ulinzi kutakuwa na ulinzi mkali nje na ndani ukiongozwa na mbwa wakali watakaokuwa wameambatana na askari kutoka kampuni ya ulinzi wa Geo Security.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia