WANAFUNZI UDOM WAMTAKA LOWASA AGOMBEE URAIS 2015

Wanafunzi zaidi ya 600 wanaosoma Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) ambao walimaliza elimu yao ya Sekondari katika shule za Kata nchini, wamemuomba Mbunge wa Monduli,Edward Lowassa kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Wawakilishi wa wanafunzi hao wapatao 40,juzi jioni walimtembelea kiongozi huyo nyumbani kwake maeneo ya Area C mjini hapa na kula naye chakula cha usiku, huku wakimueleza kuwa wapo tayari kumpigia debe, kumchangia fedha za kuchukua fomu pamoja na kuwashawishi vijana wenzao kwamba Lowassa ndiye kiongozi anayefaa kwa sasa.Hafla hiyo pia illihudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na wanafunzi hao.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia