Ticker

6/recent/ticker-posts

ANGALIA MBOWE ALIVYOENDA KUANGALIA ENEO LA TUKIO

 
DSC09341Mwenyekiti wa Chadema, Mh freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema wakiwa katika uwanja wa Soweto mchana wa leo wakati zoezi la kuchukua vipimo mbalimbali likiendelea chini ya usimamizi wa wataalamu toka Jeshini.
DSC09327
Mbowe na Lema wakishauriana jambo..
DSC09343Eneo la maafa. Inaelezwa kuwa wataalamu wa jeshi waligundua kuwako kwa kitu ndani ya tanki la mafuta na hivyo kuamua kulikata. Taarifa hizo zinadai kwamba kulikuwa na mabomu yametegwa chini ya gari na hivyo tank hilo lilishmabuliwa kwa risasi labda utokee mlipuko! Pia gari hii ya amatangazo ina majeraha mawili mlango wa kushoto yaliyotokana na kitu chenye ncha mabacho kinaweza kuwa risasi au vipande vya vyuma vya bomu.
DSC07458
DSC09360Mh Mbowe akiwa nyumbani kwa wazazi wa mmoja wa marehemu (Ramadhani) eneo la Mianzini kuwapa pole kwa kuondokewa na mpendwa wao.
DSC09382James Ole Millya na Mbunge Lema wakimjulia hali mmoja wa majeruhi walilazwa hospitali ya Seliani
DSC09373Mtoto Sharifa nae amalazwa hospitalini hapo kwa majeraha ya mlipuko
DSC09377Dereva wa mgombea wa Chadema Kata ya Themi, Bw beni akiwa majeruhi kitandani

IMG-20130616-WA0006
Kamanda wa Chadema ambaye alikuwa ni mlinzi wa amani (Red Brigade) katika mkutano huo, Bw Kitumbwizi akiugulia maumivu katika hospitali ya Selian alikolazwa baada ya kujeruhiwa katika mlipuko huo. Huyu amaumizwa mguu mmoja, mkononi na sehemu ya kwapani ambapo imegundulika kuwa kuna chuma ama risasi ndani ambayo imekuwa ngumu kutolewa mapaka sasa.

Mlipuko wa bomu uliotokea Arusha na kusababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi 70 limezua utata kutokana na hisia tofauti za viongozi mbalimbali nchini waliozungumzia suala hilo, huku Rais Jakaya Kikwete akisema haamini kama Watanzania sasa wamefikia hatua ya kuanza kuhasimiana kwa misingi ya kisiasa.
Hii ni mara ya pili kwa Jiji la Arusha kushambuliwa kwa bomu baada  ya lile lililorushwa kwenye Kanisa la Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi kwenye Parokia ya Olasiti wakati wa sherehe ya uzinduzi wake Mei 5, mwaka huu na kuua watu watatu na kujeruhi 64. Wakati Rais Kikwete akisema hayo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba wamesema tukio hilo ni la kisiasa na lilipangwa.
Kufuatia tukio hilo, uchaguzi wa  kata nne za Arusha mjini umeahirishwa hadi Juni 30.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana imeeleza kuwa Rais Kikwete ambaye yuko nchini Uingereza kuhudhuria mkutano wa nchi zilivyoendelea kiviwanda(G8), alisema haamini kama Watanzania ama wafuasi wa vyama vya siasa wanachukiana kiasi cha kudiriki kufanya matukio ambayo yanahatarisha usalama wa watu.
“Mimi   siamini   kuwa  Watanzania au wafuasi wa vyama vya siasa wanachukiana kiasi cha kufanyiana matendo ya unyama wa aina hii. Naamini kuwa hiki ni kitendo cha mtu ama watu wasioitakia mema nchi yetu, watu ambao wanatafuta kila sababu ya kupandikiza chuki miongoni mwa raia ama makundi ya raia, ili nchi yetu iingie kwenye machafuko makubwa.”
Mbowe
Akizungumzia suala hilo,  Mbowe alisema shambulio hilo la bomu ni la kisiasa na lililenga kumuua yeye na Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema.
“Haya ni mauaji ya kisiasa ya kupanga, tumeokota maganda ya risasi za bastola na SMG na tumepiga picha na kuwapa polisi katika eneo la tukio, gari letu lilipigwa mlango na vioo kwa risasi na kesho wabunge wote wa Chadema watakuwa hapa Arusha na wataondoka baada ya mazishi,” alisema Mbowe.
Mbowe alisema pia wamebaini bomu lililorushwa ni la kiwandani na shambulizi hilo liliandaliwa na kikosi cha watu wengi wenye lengo la kufanya mauaji makubwa.
Alisema kilichomwokoa na kifo ni kushuka jukwaani saa 11:43 kabla ya muda wa kawaida wa saa 12:00 kwani ilipangwa washambuliwe wakiwa juu ya jukwaa.
“Tunasikitika sana, watu wamekufa wasio na hatia na msiba huu utakuwa wa kitaifa na tunatarajia kuaga miili katika uwanja huohuo wa Soweto,” alisema Mbowe.
Profesa Lipumba

Kwa upande wake, Profesa Lipumba alisema watu waliohusika kulipua bomu walipanga kuvuruga uchaguzi huo uliyokuwa ufanyike jana.
Alisema CUF walikuwa na nguvu katika baadhi ya maeneo ya uchaguzi Arusha ndiyo mana watu wameamua kuvuruga uchaguzi  ili usifanyike.
“Sisi tumewasimamisha wagombea udiwani ambao ni Abbas Mkindi, (Kaloleni), John Bayo (Elerai) na Labora Ndarvio (Themi) na maeneo haya tulitegemea leo (jana) tushinde ila baadhi ya watu wameamua kuvuruga kwa malengo yao binafsi,” alisema Lipumba.
Katika hatua nyingine, Profesa Lipumba amevitaka vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa kina kuwabaini watu waliohusika na milipuko hiyo ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Nchimbi na Mwema
Wakati viongozi hao wakigawanyika Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi na Inspekta Jenerali wa Polisi(IGP), Said Mwema wamesema tayari jeshi lake limetuma timu inayoongozwa na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja na Kamishna wa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Isaya Mngulu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana Dk Nchimbi alisema uchunguzi wa awali umebaini ya kwamba bomu hilo ni la kurusha kwa mkono (hand grenade).
Hata hivyo, Dk Nchimbi alisema hadi sasa hakuna mtuhumiwa  yeyote anayeshikiliwa kutokana na tukio hilo.
“Uchunguzi wa awali umebaini kwamba bomu hilo ni la kutupa kwa mkono. Tunachunguza kujua mlipuko ule ni wa aina gani,” aliwaambia waandishi wa habari jijini  Arusha.
Dk Nchimbi alitaja orodha ya vifo katika tukio hilo na kusema hadi sasa watu wawili wamethibitishwa kufa, huku 70 wakiwa wamejeruhiwa ambapo kati ya majeruhi hao, wawili wako katika hali mbaya. Alisema kwamba uchunguzi huo unalishirikisha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ili kubaini mlipuko uliojitokeza ni wa namna gani.
Naye IGP Mwema alisema jeshi litaendesha operesheni kali popote nchini ya kuwasaka na kuwatia mbaroni wote waliowezesha, kufadhili na waliotenda uhalifu huo. Alisema Jeshi la Polisi linalaani tukio hilo linaloashiria vitendo vya kigaidi ambalo limesababisha vifo na majeruhi pamoja na kujenga hofu kwa wananchi.
“Nawashukuru wananchi walioanza kutupa taarifa za mwonekano, wajihi wa mtu aliyetupa bomu hilo,” alisema.
Mwema aliweka hadharani simu yake ya mkononi yenye namba 0754 785557 akitaka wananchi wenye taarifa kuhusu uhalifu huo kumpa mwenyewe taarifa au kwenye vituo vya polisi vilivyo jirani yao.

Post a Comment

0 Comments