CHANJO YATOLEWA KWA WATOTO WA MKOA WA MANYARA

Zaidi ya watoto 65,701 wenye umri wa kuanzia miezi sita hadi miaka mitano wa vijiji 65 vya Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara,wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya vitamin A na miezi 12 hadi miaka mitano watapata chanjo ya kuzuia minyoo.

Watoto hao watapatiwa chanjo hiyo,sehemu tofauti ikiwemo vituo vya afya na zahanati za Serikali na za binafsi na lengo la chanjo hiyo ni kutokomeza vifo vya watoto chini ya umri huo ifikapo mwaka 2015. 

Mkuu wa wilaya ya Hanang’ Christina Mndeme,akizungumza wakati akizindua chanjo hiyo juzi kwenye kijiji cha Hirbadaw,alisema jamii inatakiwa kuwapeleka watoto wao kupata chanzo hiyo ili kudhibiti magonjwa hayo ya watoto.

Mndeme aliitaka jamii kushiriki kikamilifu kwa kuhakikisha watoto wao wanapatiwa chanjo hiyo na kuepukana na dhana potofu kuwa chanjo hiyo ina madhara kwa watoto wao.

“Serikali inawapenda sana wananchi wake ndiyo sababu imetumia fedha nyingi kugharimia chanjo hizi,hivyo msiwasikilize wale wote wanaoeneza fikra potofu juu ya chanjo hizi ambazo watoto wanapatiwa,” alisema Mndeme.

Alisema wazazi wanaowapeleka watoto wao kwenda kupata chanzo hizo wanapaswa kuwashawishi wenzao kuwapeleka watoto wao kupata chanjo hizo katika vituo vya afya na zahanati zilizo karibu na sehemu wanazoishi.

Watoto wanaotarajiwa kupata chanzo hiyo hapa nchini,ni zaidi ya 202,560 ambapo inadaiwa kuwa watoto zaidi ya 15,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na maradhi mbalimbali.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia