Ticker

6/recent/ticker-posts

DIWANI AMWAGA CHOZI JUKWAANI KATIKA KATA YA ELERAI

Uchaguzi wa udiwani kwenye jimbo la Arusha umechukuwa sura mpya baada ya mgombea wa udiwani wa chama cha wananchi (CUF)kwenye kata ya Elerai John Gilbert Bayo kuangua kilio jukwaani wakati akinadi sera zake mbele ya wananchi, wakazi wa kata hiyo na katibu mkuu wa chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad.
 
Mgombea huyo aliangua kilio hicho baada ya kuwaambia na kuapa mbele ya wakazi hao wa kata yake kuwa hakuwahi kupokea fedha kiasi cha 50 milion kwa ajili ya kupata muafaka wa meye wa jiji la Arusha kama chama cha demokrasia na maendeleo wanavyodai na kuwa hata weza kukiuka maadili na kuwatosa waliomchagua.
 
Akizungumza kwenye kampeni hizo katibu mkuu wa CUF na makam wa kwanza wa serekali ya umoja wa kitaifa ya Zanzibar Seif Sharif Hamad aliwataka wakazi wa kata ya Elerai kuwachagua wagombea wa chama hicho kwani chama hicho kimekuwa kikihimiza umoja na Amani wakti wote.
 
Maalimu Seifu akabainisha kuwa Mgombea wa CUF kwenye kata ya Elerai John Bayo ni mtu makini na mchapakazi na kuwa wao hawapo kumfukuza mtu bali wananchi ndio watakao amua hatma ya viongozi wanaowataka kwani sisi CUF ndio walimu wa amani hapa nchini kama tungekuwa hatuhubiri amani Zanzibar isinge kalika baada ya uchaguzi mkuu kwani chaguzi zote tuliweza kushinda lakini tulipokwa ushindi.
 
“Sisi CUF ndio wahubiri wa amani kwani tangu mwaka 1995 tumeshinda chaguzi zote lakini kwa hekima na busara tuliwakataza vijana kuingia barabarani kudai haki yao lakini leo matunda ya busara si mnayaona”alisema Maalimu Seifu.
 
Zanzibar wananchi waliishi kwa uhasama na tukaona kama tutaenda hivyo kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 basi kutaweza kutokea mchafuko hivyo mimi na Rais mstaafu Karume tulikaa na baaadae vyama na hatimaye wananchi zaidi ya 66%akaidhinisha muafaka huu ni uamuzi wa busara na leo ndiyo iliyozaa serekali ya umoja wa kitaifa.
 
Maalimu akatanabaisha kuwa CUF inaimani na John Bayo kwa kuwa ndiyo chaguo la wananchi wa kata hiyo na kuwataka kumpa kura zote iliawe diwani wao na kusema hivi sasa Zanzibar imetulia baada ya mwafaka ule na haya ni matunda ya chama hicho na kuwa hawatajuta kuchagua mgombea wa chama hicho kwenye kata zote waliosuimamisha wagombea.
 
Naye mgombea wa udiwani wa Kata ya Elerai John Bayo alisema kuwa akichaguliwa atapambana na kero mbalimbali zinazowakabili wakazi wa kata hiyo ikiwemo kutoa michango ya kununua madawati na majembe kila mwaka kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.
 
Bayo akawataka wakazi wa kata hiyo kuwaonyesha kuwa hakuchaguliwa na mafuriko ya chadema kwa kumpigia kura ya ndiyo kwenye uchaguzi huo siku ya tarehe 16 mwezi huu na kuwa majengo ya Zahanati wao hawataki zahanati bali kituo cha Afya hivyo wakimpa ridhaa hizo zitakuwa kipaumbele chake

Post a Comment

0 Comments