Ticker

6/recent/ticker-posts

WADAU 40 WA SEKTA YA FEDHA KUTOKA NCHI NANE ZA JUMUIYA ZA MADOLA WAPATIWA ELIMU


Zaidi ya wadau 40 wa sekta ya fedha kutoka nchi nane za jumuiya ya madola wanapatiwa mafunzo ya teknolojia mpya ya udhibiti na ukopaji wa madeni ya nje ili kuweza kuthibiti madeni na ukopaji kwenye nchi zao.
 
Semina hiyo ya wiki mbili pamoja na hayo pia watabadilishana uzowefu katika nyanja za kifedha kutoka kwenye mataifa yalioendelea na nchi zinazoendelea inayofanyika kwenye jiji la Imeelezwa ya kwamba vijana wengi nchini hawana uelewa wa elimu ya uraia hali ambayo imepelekea baadhi yao kushindwa kutambua majukumu yao ya msingi na fursa mbalimbali za kuwaingiza kipato.

Hayo yalisemwa hivi karibuni na katibu wa asasi isiyo ya kiserikali ya Mategemeo Women Association,Viola Likindikok  wakati alipokuwa akizungumza katika mdahalo wa elimu ya uraia ulioandaliwa na asasi hiyo .

Mdahalo huo uliwashirikisha zaidi ya vijana 100 kutoka kata za Lemara na Daraja mbili ambapo miongoni mwao ni wanafunzi wa shule za sekondari zilizopo ndani ya kata hizo.

Katibu huyo alisema kwamba katika utafiti wao wamebaini ya kwamba vijana wengi nchini hawana elimu ya kutosha kuhusu suala la uraia hali ambayo imekuwa ikichangia kushindwa kujitambua.

Hatahivyo,alisisitiza ya kuwa  katika midahalo mbalimbali waliyoifanya vijana wengi wamekuwa wakihoji kuhusu suala la ajira ambalo alikiri ni changamoto kuu kwa serikali na kila mdau wa maendeleo  hapa nchini.

Naye,mkuu wa kitengo cha polisi jamii mkoani Arusha,Mary Lugola alisema ni vyema vijana nchini wakapewa elimu ya uraia ili waweze kujitambua na kuepuka kutumiwa katika harakati mbalimbali za kichochezi.

Baadhi ya watoa mada katika mkutano huo,Happy Mwajunga na Salmin Sulle walisema kuwa waliwataka vijana kuacha kulalamika na kukata tamaa katika maisha huku wakiwasisitiza kuwa wadadisi ili waweze kutambua fursa mbalimbali za kuwaingizia kipato.

Post a Comment

0 Comments