Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS KIKWETE AZINDUA UJENZI WA BARABARA YA MAGOLE-TURIANI-MZIHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya akiweka jiwe la Msingi kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani –Mziha sehemu ya Magole-Turiani (48.6km) inayojengwa kwa kiwango cha lami.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, mbunge wa Mvomero Amos Makalla, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani (48.6km



Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale akitoa maelezo ya kina kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km)


Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wa kwanza kulia akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe kabla ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani (48.6km) kwa kiwango cha lami

Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya wakifurahia jamabo na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mheshimiwa Antony Mtaka kabla ya uzinduzi  wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiwa pamoja na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kushoto wakifurahia kikundi cha ngoma za asili mara baada ya Mheshimiwa Rais kuwasili Wilaya ya Mvomero kwa ajili ya kuzindua ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km)



Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe wa kwanza (kushoto) akizungumza kabla ya uzinduzi rasmi wa barabara ya Magole Turiani. Wa kwanza kulia kwake ni Mkurugenzi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi Mhandisi Ndyamukama pamoja na Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi na Umeme Dkt. Wiliam Nshama

Sehemu ya Matengenezo ya Daraja katika barabara ya Barabara ya Magole-Turiani (48.6km)

Post a Comment

0 Comments