Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu kamishna (DCP) Charles Mkumbo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari juu ya jambazi hilo lililowawa
Na Woinde Shizza,Arusha
Mtu mmoja anayesadikiwa kuwa ni
jambazi alijeruhiwa kwa kupigwa risasi na askari Polisi kisha kufariki dunia
wakati akipelekwa katika hospitali ya Monduli kwa ajili ya matibabu.
Akithibitisha kutokea kwa tukio
hilo alipoongea na waandishi wa habari leo mchana ofisini kwake, Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Arusha,Naibu Kamishna
(DCP) Charles Mkumbo alisema tukio hilo lilitokea muda saa 07:00 Usiku maeneo
ya Makuyuni barabara ya Arusha-Makuyuni wilayani Monduli.
Kamanda Mkumbo alisema jambazi
huyo akiwa na wenzake wapatao 29 walikuwa na bunduki ambayo bado haijafahamika
pamoja na silaha za jadi mapanga na marungu ambapo waliweka mawe barabarani na kulisimamisha
gari aina ya Fusso lenye namba za usajili T. 871 BUZ ambalo lilikuwa lina mzigo
likitokea Moshi kuelekea mkoani Singida.
‘’Mara
baada ya kulisimamisha gari hilo wakaanza kumpora abiria mmojawapo
aliyejulikana kwa jina la Victor Pius (46) Mfanyabiashara, mkazi wa Majengo Moshi
ambapo walichukua simu mbili aina ya Nokia na Samsung pamoja na fedha taslimu
Tsh 50,000/=’’.
“Wakati
wanaendelea na tukio hilo askari Polisi waliokuwa High Way Patrol walipata
taarifa za tukio hilo ambapo walikwenda kwa haraka na mara baada ya majambazi
hao kuwaona walianza kufyatua risasi hovyo na Polisi kuanza kujibu mapigo na
kufanikiwa kumjeruhi mmojawao na kuwakamata wengine kumi na mbili papo hapo
wakiwa na mapanga sita na marungu manne huku wengine akiwemo na yule mwenye
bunduki wakikimbia”. Alifafanua Kamanda Mkumbo.
Kamanda
Mkumbo alitoa wito kwa wananchi wa mkoa huu kuendelea kushirikiana na Jeshi la
Polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu ili zifanyiwe kazi kwa haraka, huku akitoa
onyo kwa majambazi wanaopenda kujipatia kipato bila kuvuja jasho kwani Jeshi
hilo limejiandaa vizuri.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia