CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo mkoa wa Arusha(CHADEMA)kimesema kuwa kinatarajia kumfungulia mashitaka mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo dhidi ya kauli zake za uchochezi dhidi ya Chama hicho lakini pia kauli za vitisho kwa Mbunge Lema ambaye kwa sasa anashikiliwa na Polisi.
Akizungumza na vyombo vya habari mapema jana Katibu wa chama hicho Amani Golugwa alisema kuwa zoezi hilo lipo mbioni kukamilika kwa kuwa wanasheria wa chama hicho tayari wameshapewa taarifa hizo
Golugwa alisema kuwa Magesa Mulongo amekuwa kikwazo kikubwa sana kwa kuwa sio mara ya kwanza kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Chadema lakini hata mara nyingine amekuwa akimtuhu Lema kwa uongo uongo hali ambayo hadi kwenye mauaji ya chuo cha uasibu ilijitokeza
Aliendele akwa kusema kuwa kama wataweza kupuuzia hali hiyo itazidi kuwaumiza sana na ikubambikiwa kesi ambazo si za kwao kama hali ilivyo kwa sasa ambapo kuna dalili za Mbunge Lema kubambiwa kesi ya mauaji yaliyotokea katiika chuo cha Uasibu
“tunavyoongea mpaka sasa tayari tumeshawasiliana na wenzetu ambao ni wanasheria wa Chadema na tutamfikisha mahakamani huyu Mkuu ili iwe fundisho kubwa sana manake kauli zake za uchochezi na za kutupinga sisi zinatuchosha sana na mimi kama Katibu naona amefilisika kisera na hata kimawazo kwa kuwa kamwe siwezi mfananisha hata na mtendaji wangu wa chama”aliongeza Golugwa
Akiongelea Kesi inayomkabili Mbunge Lema alisema kuwa mpaka sasa mlalamikaji katika kesi hiyo hakuna lakini vitisho alivyotoa mkuu huyo wa mkoa vinasema kuwa Lema kwa sasa hatabanduka na wala hatachomoka hali ambayo ni fedheha tu lakini wao kupitia kwa mwanasheria wao wanajopanga vilivyo kukabiliana na Mkuu huyo wa mkoa
Awali Wakili wa Mbunge Lema ambaye ni Bw Humprey Mtui alisema kuwa anashangazwa na kitendo cha jeshi la polisi kumvunjia hesima mbunge Lema na badala yake kumfanya kama Kapurwa mtaani kwa shinikizo la maslahi ya watu wacheche
Alisema kuwa kwa mujibu wa sheria Lema angepswa kuitwa na Polisi lakini kama angetaa basi ndio angeweza kuchukuliwa sheria kama hiyo lakini sio kwa kitendo cha polisi walichokifanya cha kuvuka ukuta wa nyumba ya mbunge huyo
Bw Mtui alisema kuwa mbali na hayo pia hata haki za msingi kama vile kuswaki na kunywa chai mbunge huyo ananyimwa na Polisi jambo ambalo ni ukiukaji mkubwa sana wa Sheria ya Maabusu hapa Nchini ukilinganisha kuwa yeye bado ni mbunge na tena mwakilishi wa wananchi
Alifafanua kuwa bado watakuwa na mbunge huyo na wataweza kufuata sheria za msingi lakinii kwa wale wote ambao wanamuonea Mbunge huyo watachukuliwa sheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani kwani hali za uoneaji dhdi yake zinaongezeka siku hadi siku.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia