Ticker

6/recent/ticker-posts

KUWENI NA MSHIKAMANO ,UPENDO ILI KUDUMISHA AMANI ASEMA OGORI

Jamii nchini imetakiwa kuwa na mshikamano upendo na kudumisha amani iliyopo ambayo imeachwa na waasisi wa Taifa la Tanzania bila kujali dini,kabila wala itikadi au ubaguzi wa aina yoyote ile.

Hayo yalielezwa juzi na Mwenyekiti wa kikundi cha Muungano cha Mji mdogo wa Mirerani Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,Daudi Ogori baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo.

Ogori alisema watanzania wanapaswa kuendeleza amani na upendo uliopo nchini,ambayo ni tunu iliyoachwa na waasisi wa Taifa kuliko kuendeleza chuki na mifarakano ambayo haina sababu za msingi.

Katika uchaguzi huo Ogori alichaguliwa kuwa Mwenyekiti kwa kupata kura 196 dhidi ya Odianya Suke aliyepata kura 158 na Makamu Mwenyekiti alishinda Msiem Ondere aliyepata kura 200 na Gay Abiti alipata kura 120.

Nafasi ya Katibu mkuu,ilikamatwa na Mtaalam Nyang’ore aliyepata kura 200 dhidi ya Fred Oguti aliyepata kura 120 katika uchaguzi huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa.

Wakizungumza baada ya kupata nafasi hizo,viongozi hao waliwashukuru wanachama wa kikundi hicho kwa kuwapa nafasi hizo na waliahidi kutumika kwenye nafasi hizo kadiri ya uwezo wao.

Walisema kuongoza ni dira hivyo nao watatumia nafasi hiyo kwa ajili ya kuongoza kikundi hicho na jamii kwa ujumla huku wakitanguliza mbele maslahi ya wanakikundi waliowapa dhamana kubwa ya kuwachagua.


Post a Comment

0 Comments