Ticker

6/recent/ticker-posts

CHADEMA ARUSHA WALIA KUKODEKANA KWA MKURUGENZI WA KUDUMU WA HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA

jenerali
 
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) mkoani Arusha kimelalamikia kitendo cha uongozi wa halmashauri ya jiji la Arusha kukosa mkurugenzi wa kudumu katika ofisi hiyo kwa takribani miaka mitatu hadi sasa.
Hadi sasa halmashauri ya jiji la Arusha haina mkurugenzi kamili baada ya aliyekuwa kaimu wake,Omary Mkombole kuhamishiwa wilayani Babati kuwa mkurugenzi kamili na kwa sasa inakaimiwa na mhandisi mkuu,Afwilile Lamsy.
Akitoa tamko hilo juzi mwenyekiti wa madiwani wa Chadema jijini hapa,Isaya Doita alisema kuwa inashangaza ofisi ya jiji hilo kukaimiwa kwa miaka mitatu hadi sasa bila kuwa na mkurugenzi kamili.
Alisema kuwa cha ajabu ofisi ya mkurugenzi wa jiji la Arusha imekuwa ikitumiaka kuandaa wakurugenzi mbalimbali wanaopitia Arusha na kwenda kuwa wakurugenzi katika maeneo mengine nchini.
Doita,ambaye pia ni diwani wa kata ya Ngarenaro jijini hapa alitolea mfano wa makaimu wakurugenzi ambao wamepitia jijini hapa na kwenda kuwa wakurugenzi kamili ni pamoja na mkurugenzi wa halmashauri ya Mpanda,Estomi Chang”a sanjari na mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati,Mkombole.
“Tunapinga kitendo cha halmashauri yetu kutumika kama kituo cha kuandaa wakurugenzi wanaopelekwa katika maeneo mengine nchini ihali sisi tunabaki na makaimu tu”alisema Doita

Post a Comment

0 Comments