Ticker

6/recent/ticker-posts

MASHIRIKA 13 YASIYOKUWA YA KISERIKALI YAMSHUKIA KAGASHEKI ATAKIWA KUACHA KUPOTOSHA UMMA WA WATANZANIA JUU YA MGOGORO WA ARDHI WA LOLIONDO

DSCF8645
Mkurugenzi wa shirika la PINGO’S Edward Porokwa akisoma tamko kwa wanahabari  jijini Arusha tamko lililoshirikisha mashirika 13 yasiyokuwa ya kiserikali juu ya mgogoro mkubwa wa ardhi unaondelea Loliondo
DSCF8646
DSCF8644
DSCF8648
Jovitha Mlay kutoka (TGNP)aliyevalia nguo nyekundu alisoma tamko kwa wanahabari
DSCF8653
Onesmo Olengurumwa Mtetezi wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania(THRD)akisoma tamko
MASHIRIKA yasiyo ya kiserikali 13 hapa Nchini wanaotetea haki za binadamu kwa pamoja wametoa tamoko lao kuhusu mgogoro mkubwa wa ardhi unaoendelea Loliondo dhidi ya mwekezaji OBC  huku wakimtaka Waziri wa mali asili na utalii kuacha kupotosha umma wa watanzania juu ya mgogoro huo
Hatua hiyo imekuja baada ya hivi karibuni waziri wa mali asili na utalii Mh.Balozi khamisi Khagasheki kutoa taarifa kwa umma kupitia vyombo vya habari kuwa serikali imeamua kupunguza ukubwa eneo hilo ili kutatua migogoro  iliyopo  katika eneo hilo kunusuru ikolojia ya hifadhi ya Serengeti,Ngorongoro na Pori tengefu la Loliondo
Watetezi hao kwa pamoja walitoa tamko hilo jijini Arusha tarehe 4/4/2013 ambapo Mkurugenzi wa shirika la PINGO’S Edward Porokwa akisoma tamko kwa wanahabari alisema kuwa upotoshaji huu umekuwa na lengo la kuwaahadaa umma wa Watanzania na ulimwengu kwamba eneo lote la loliondo ni eneo la hifadhi pekee na siyo ardhi ya vijiji hivyo wananchi kuonekana ni wavamizi jambo ambalo si lakweli
Alisema kuwa  nia ya serikali kuwaondoa wananchi katika maeneo yao ya vijiji vyao kumekuwepo na hatari kubwa ya wizara kutumia mbinu za kumega na kupokonya kilomita za mraba 1500 ya ardhi ya vijiji na kuikabidhi kampuni ya OBC kwa kisingizio cha kuwagawia sehemu ya pori tengefu la loliondo huku akidai kuwa siyo sahihi kwa kuwa ni ya vijiji husika
“Wanahabari  Ardhi ambayo Serikali inasema imewaachia wananchi ni ardhi ya vijiji vilivyopo katika mipaka na katika hili, Serikali imepokonya ardhi yenye ukubwa wa kilometa za mraba 1,500 na kumpatia mwekezaji wa OBC”alisema
Kwa upande wake , Jovitha Mlay kutoka (TGNP)alisema kuwa uamuzi wa serikali wa kugawa eneo la vijiji na kulifanya kuwa pori tengefu unachochea mgogoro uliopo kwa sasa  huku akisisitiza kwamba siyo kweli kuwa serikali ina lengo la kuinusuru ikolojia ya hifadhi ila nia yake ni nikumpatia mwekezaji OBC.
“Hii haina ukweli wowote kwani serikali wasingeruhusu uwindaji ufanyike kama wangekuwa na uchungu wa kuwalinda wanyama pamoja na ikolojia hiyo”alisema Mlay
Naye Mtetezi wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania Onesmo Olengurumwa alisema kuwa serikali iache mara moja mpango wake wa kugawa ardhi ya wananchi kwa manufaa ya mwekezaji kwa kisingizio cha manufaa ya umma
“Naomba serikali iache mara moja kuptosha umma kuwa ardhi hiyo siyo ya vijiji na izingatie sheria kwa kuvipa vijiji haki ya kuamua mambo yao kwa kuzingatia sheria za serikali ya mitaa”
Mashirika hayo yaliyotoa tamko ni PINGO’S Forum,TALA,Haki Ardhi,LHRC,Tanzania human Rights Defendes,TGNP,TNRF,Cords,CRT,PWC,NGONET,TPCF,OSEREMI

Post a Comment

0 Comments