Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS ATEUWA BODI MPYA YA KAHAWA TANZANIA

Mmoja wa wajumbe wa bodi mpya ya Kahawa walioteuliwa  Meynard Swai ambaye pia ni Meneja wa KNCU.




Rais Jakaya Kikwete amemteua Bibi Eze Hawa Sumari kuwa mwenyekiti mpya wa bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) kuchukua nafasi ya Pius Ngenze.

Ngeze amekuwa mwenyekiti wa bodi hiyo tangu mwaka 2008 hadi Desemba mwaka jana ambapo bodi yake ilimaliza muda wake wa uongozi

Tayari Ngeze na wajumbe wengine waliomaliza muda wao wameagwa rasmi na watumishi wa bodi hiyo katika hafla iliyofanyika February 27,2012

Sanjari na mwenyekiti huyo pia waziri wa kilimo,chakula na ushirika Prof Jumanne Maghembe ameteua wajumbe wapya watakaounda bodi hiyo.

Wajumbe hao ni pamoja na Fatuma Faraji ,Novatus Piigererwa, Yasinti Ngwasura na Eric Ng'maryo.

Wengine ni Maynard Swai ambaye ni Meneja wa KNCU,Prof James Terri ambaye ni mkurugenzi wa kituo cha utafiti wa zao la Kahawa(Tacri),Mh John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga na Eng Merad Omar Msuya.

Post a Comment

0 Comments