Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS AWASILI MKOANI KIKWETE KILIMANJARO WA ZIARA YA SIKU TATU

 Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya  Mrisho Kikwete akiwa amewasili mkoani Kilimanjaro apa alikuwa anasalimia na baadhi ya viongozi wa mkoa huo
 wanawake wa mkoa wa Kilimanjaro walijitokeza kumpokea Rais huku kila mmoja akionekana akiwa na uso wa furaha
 Raisi alipokelewa na vikundi vya ngoma za asili hapa alikuwa anaangalia wakicheza
 Mwenyeji wa ugeni huu ambaye ni mkuu wa mkoa wa |Kilimanjaro Leonidas Gama akiwa anawapa wageni wake histori fupi ya mkoa


Miongoni mwa shughuli ambazo Mheshimiwa Rais atafanya ni pamoja na kuzindua kampeni ya kupinga ukatili na matumizi ya nguvu dhidi ya wanawake ambayo ataizindua kwa kuanzisha safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro iliyopewa jina la “Kilimanjaro Speak Out, Climb Up”.
 
Shughuli hiyo itakayofanyika leo Jumatatu, Machi 5, 2012 asubuhi, imepangwa kwenye Lango la Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA)
Mbali na kuanzisha kampeni hiyo, Mhe Rais pia atafungua Mkutano wa Mwaka wa Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika kwenye Chuo cha Polisi mjini Moshi.
 
Hii ni ziara ya kwanza ya Mhe Rais Kikwete katika Mkoa wa Kilimanjaro tokea alipotembelea Mkoa huo wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
 
 

Post a Comment

0 Comments