MWALIMU AFARIKI NA AJALINYA PIKIPIKI

Mwalimu wa shule ya sekondari Musa afa kwenye ajali ya pikipiki eneo la kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha wakati akiendesha pikipiki yake aina ya Honda yenye namba za usajili T164BAA baada ya kugongwa na gari huko kisongo.

Akizungumza na vyombo vya habari kamanda wa polisi mkoani hapa kamishna msaidizi wa polisi Liberatus Sabas alisema kuwa Mnamo majira ya usiku huko maeneo ya kisongo barabara ya Dodoma gari lenye namba za usajili T647AQH aina ya RAV4 iliyokuwa ikiendeshwa na Lambert Teuwissen miaka32 raia wa Holland mkazi wa moshono alimgonga mwendesha pikipiki na kusababisha mauti ya mtu huyo.

Kamanda Sabas alisema kuwa mtu huyo alitambuliwa kuwa ni mwalimu wa shule ya sekondari musa aliyopo kisongo na katika hatua nyingine siku hiyo hiyo huko maeneo ya Ilbouru gari namba T231CAR aina ya TOYOTA hiece iliyokuwa ikiendeshwa na dereva asiyefahamika ilimgonga mwendehsa piki piki na kusababisha mauti wa abiria wa pikipiki hiyo.

Pikipiki hiyo yenye usajili no.T138CBJ iliyokuwa ikiendeshwa na Sadiki Athman miaka 20 ilipata ajali na kusababisha kifo cha Maliki Bakari(23)ambaye alikuwa abiria wa pikipiki hiyo huku dereva akipata majeraha sehemu mbali mbali za mwili wake.

Kamda Sabas alisema kuwa anatoa wito kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto na vya usafiri kuchukuwa tahadhari na kuwa makini kwa kuzingatia kanuni na sheria za usalama barabarani ilikuepuka matukio ya ajili .

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia