Ticker

6/recent/ticker-posts

CHIKU K “NAMPENDA SANA CHID BEENZ NA TUMEYAMALIZA YA ZAMANI NIKO NAYE KWA SASA NA NITAMBADILISHA”

CHIKU
CHIKU K
Mwanadada Chiku Ketto a.k.a Chiku K Balaa ameamua kuweka wazi hisia zake alizonazo kuhusu kile anachokiona kinamtesa Aliyekuwa Member Mwenzake wa Kundi la LaFamilia.
Akizungumza na Kipindi cha DUNDO cha MamboJambo Radio Arusha kupitia Kipengele cha DROP BOX Chiku amesema ana mpango wa kukaa Karibu zaidi na Chid Beenz Kwakuwa anajua anakoelekea sio kwema kwani wakati wakiwa Pamoja Chid alikuwa na Mafanikio na Hakuwa kama alivyokuwa Kitu ambacho kinaonekana kama Chid beenz amekosa mtu wakuwa karibu zaidi na yeye kwa Ushauri na Ukaribu wa Kimawazo Chanya.
Bila shaka mmefuatilia pia Kesi ambayo ilikuwa inamkabili Chid Beenz ambayo ilikuwa ya Kukutwa na Madawa ya Kulevya Katika Uwanja wa JK Nyerere Airport na kuachiwa huru kwa Faini ya sh. 900 000/= za Kitanzania Hivi juzi hii ni moja ya sababu zinazoonyesha Chid Baanz amefikia kubaya zaidi.
UKIWA unakumbukumbu nzuri sana utakumbuka wakati ule chid akiwa na LaFamilia Team yake hata kiafya alikuwa Kajaza na hata watu walikuwa wanamuogopa kwa kuwa alikuwa na Lile Body Flani la Kinako ila kwa sasa hata machalii wanweza kumchezea Japo Wembamba hauna maana ya kuwa Umeisha na nguvu ila kiukweli Chid Amepungua sana Kiafya.
Chid Beenz_full (1)
CHID BEENZ ENZI HIZO
CHIDBENZ
CHID BEENZ KWA SASA
Chiku amemshauri Chid Kuhakikisha Anakumbuka kuna Mama yake, Ndugu zake Wanamtegemea na pia Jamii nzima inamwangalia na Cha Mwisho akasema anampenda sana Chid Beenz Kuna ngoma wamefanya kwa Pamoja na Atahakikisha Kuwa Chid anaepukana na Majanga yanayomwandama.
 
Katika Mazungumzo hayo Chiku amepata Pia nafasi ya Kuzungumzia Ngoma zake Mbili ambazo zinatoka mwisho wa Mwezi huu au mwanzoni mwa mwezi ujao Ambapo ngoma hizo mojawapo ni PIGA HATUA ambayo ilikuwa itoke mwaka jana Mwishoni lakini ikashindwa kutoka sababu alizozitaja kuwa ni Matatizo yaliyokuwa yametokea katika Management yake na Ya Pili ni ngoma ambayo itakuwa inahamasisha Vijana Kupiga Kura Ukizingatia huu ni mwaka Muafaka kwa Watanzania Kumchagua Rais Mpya, Wabunge na Madiwani katika Serikali Kuu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Post a Comment

0 Comments