Ticker

6/recent/ticker-posts

BBC MEDIA ACTION WAWAPIGA MSASA WAFANYAKAZI WA RADIO 5




???????????????????????????????
Wafanyakazi wa kampuni ya Tan Communication Media  inayo miliki kituo cha  Radio 5 chenye makao yake makuu jijini Arusha wakiwa katika picha ya pamoja jana katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kitaaluma ili waweze kuandika habari za kuboresha maisha ya jamii kwa kupata maendeleo kuelekea uchaguzi mkuu,mafunzo hayo yanaendeshwa na shirika lisilo la kiserikali la BBC Media Action, aliyevalia shati la blue ni mkufunzi mwandamizi Pendael Omari wa shirika hilo
???????????????????????????????
Mkufunzi mwandamizi Pendael Omari wa shirika lisilo la kiserikali la BBC Media Action akiwa anatoa ufafanuzi katika mafunzo hayo yaliyokuwa yakifanyika katika ofisi za Radio 5,mafunzo hayo yalidumu kwa takribani wiki mbili
???????????????????????????????
Mtangazaji maarufu wa kituo hicho Ernest Matundiro a.k.a Prince de la ville kushoto akiwa anaandika vipengele muhimu katika uandishi wa habari,kulia ni Mhariri wa kituo hicho Monica Nangu
???????????????????????????????
Msimamizi mkuu wa vipindi vya Radio 5  kulia Mathew Philip akiwa anafatilia mafunzo kwa ukaribu zaidia,kushoto ni mtangazaji wa kituo hicho Wilberd Kiwale
 
 
Wafanyakazi wa Radio 5 jijini A rusha wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kitaaluma ili waweze kuandika habari za kuboresha maisha ya jamii kwa kupata maendeleo kuelekea uchaguzi mkuu,mafunzo hayo yanaendeshwa na shirika lisilo la kiserikali la BBC Media Action,

Akizungumza  katika mafunzo hayo Mkufunzi mwandamizi Pendael Omari wa shirika lisilo la kiserikali la BBC Media Action alisema kuwa lengo la kufanya mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wa kitaaluma pindi wanapokuwa katika kazi zao

Alisema kuwa mafunzo hayo yatawezesha pia upatikanaji wa utawala bora kwa kuwa vyombo vya habari vitaelimisha wananchi umuhimu wa kuchagua viongozi watakaoleta maendeleo

Kwa  upande wake Msimamizi mkuu wa vipindi vya radio hiyo  Mathew Philip  alisema kuwa mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa kufanya kazi kwa kuwa walikuwa wakifanya mafunzo kwa vitendo zaidi 

Pia alisema kuwa kupitia mafunzo hayo wamepata ufahamu wa namna ya kutafuta habari za kupigia kura maoni pamoja na uchaguzi mkuu bila upendeleo kwa kumpa msikilizaji nafasi ya kusikika na kumpa elimu

Post a Comment

0 Comments