Ticker

6/recent/ticker-posts

RUSHWA,UFISADI VINAKWAZA UCHUMI WA AFRIKA-;DKT BILAL

Makamu wa Rais,Dk Mohammed Billal amesema ya kwamba  matatizo  ya rushwa na ufisadi katika baadhi ya nchi barani Afrika yamechangia kudumaza uchumi na hata kuwatisha wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali ya nje kuwekeza barani Afrika na kutoa wito kwa wakuu wa nchi hizo kupiga vita changamoto hizo.

Billal,alitoa kauli hiyo  wakati akifunga kongamano la tatu la viongozi vijana barani Afrika ambapo zaidi ya vijana 400 kutoka Afrika na China walishiriki kongamano hilo mkoani hapa.

Akifunga kongamano hilo makamu huyo wa Rais alisema kwamba baadhi ya nchi za Afrika zimeshindwa kupiga hatua kiuchumi kutokana na vikwazo vya rushwa na ufisadi.

“Rushwa na ufisadi bado ni tatizo kubwa barani Afrika kwani baadhi ya nchi uchumi wake umeshindwa kukua kutokana na changamoto hii”alisema Bilal

Hatahivyo,alisema kuwa mbali na rushwa pia matatizo ya uongozi dhaifu,utawala wa kimabavu,ukabili sanjari na kuminywa kwa demokrasia kumechangia baadhi ya wawekezaji kutoka mataifa ya nje kushindwa kuwekeza Afrika.

Awali akitoa shukrani zake kwa wajumbe mbalimbali katika mkutano huo,mwenyekiti wa Uvccm mkoani Arusha,Robinson Meitinyiku alisema kuwa ni muda wa bara la Afrika kwa pamoja kupinga ukandamizaji unaofanywa na  mahakama ya kimataifa ya kesi za jinai (ICC).

Alisema kuwa  kitendo cha wakuu wa nchi Afrika kupitia mkutano wao  uliofanyika nchini Ethiopia hivi karibuni kupinga udhalilishaji wa mahakama hiyo kwa viongozi waliopo barani Afrika ni kitendo cha kijasiri na kinapaswa kuungwa mkono na bara zima la Afrika.

“Kazi iliyofanywa na viongozi wetu wa Afrika kupitia mkutano wao ilikuwa nzuri kwa kuwa kwa pamoja walipaza sauti kupinga ukandamizaji wa mahakama hii ya ICC”alisema mwenyekiti huyo na kuibua shangwe kwa wajumbe wa mkutano huo

Naye,katibu mkuu wa chama cha Kikomunisti cha China,Zhou Changkui akitoa shukrani zake alisema kuwa China itaendelea kushirikiana bega kwa bega na Tanzania katika kuhakikisha  wanawasaidia vijana mbalimbali walipo katika nchi hizo mbili hususani katika sekta ya ajira.
 

Post a Comment

0 Comments