Ticker

6/recent/ticker-posts

AJINYONGA KWA KATANI


Mtu mmoja amefariki dunia mara baada ya kujinyonga na watu wawili wamekamatwa wakiwa na misokoto ya madawa ya kulevya 314.

Akithibitisha kutokea kwa matukio hayo  kamanda wa polisi mkoani hapa alisema kuwa tukio lakwanza lilitokea maeneo ya Engoserngiu katika halmashauri ya jiji la Arusha ambapo mtu aliyejulikana kwa jina la Bw. Tisiano Likiwilike(30) makazi wa Engosengui alikutwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya manila ambapo 8ilifungwa kwenye mti uliopo pembeni mwa nyumba aliyokuwa anaishi.

Alisema kuwa uchunguzi wa awli wa polisi umebainishwa kwamba siku ya tarehe 20 muda wa saa 11:jioni marehemu aliondoka nyumbani kwake bila kuaga na kuelekea kusiko julikana na tarehe 21 muda huo wa saa 2:30 asubui  baadhi ya mashuhuda waliukuta mwili huo umeninginia juu ya mti.

Alibainisha kuwa mashuhuda waliamua kutoa taarifa katika kituo kikuu cha polisi ambapo askari waliokuwa doria maendeo ya karibu  na tukio hilo na walipofika eneo la tukio waliukuta mwili huo na walipofanya uchunguzi katika chumba cha marehemu walikuta karatasi juu ya kitanda chake iliyoandikwa ujumbe usemao asilaumiwe mtu yeyote juu ya kifo changu kwani maisha n ya duniani yamenishinda sina thamani tena.


Kamanda amesema umeifadhiwa katika chumba cha kuifadhia maiti cha Mounti  meru  kwa ajili ya uchunguzi zawa daktari na jshi la polisi mkoani hapa linaendelea na upelelezi wa tuki hilo.

Wakati huo huo watu wawili wamekamatwa na madawa ya kulevya  aina ya baingi 314 latola eneo la unga Limited lililopo katika halmashauri ya jiji la Arusha .

Aliwataja watu hao waliokamatwa kuwa ni Bi. Linah Christop pamoja na Elizabety Chirstoph ambao walikutwa na misokoto hiyo  katika eneo la soko mjinga Ungalimeted


Alibainisha kuwa mafanikio hayo yalitokana na taarfa zilizotolewa na raia mwema kwa jeshi la ambapo mara baada ya taarifa hiyo askari hao walikenda moja kwa moja katika nyumba ya watuhumiwa na kupekuwa ndipo walifanikiwa kupata bangi hiyo iliyokuwa imehifadhiwa kwenye mfuko wa Plasitikc maarufu kama Malboro

Alibainisha kuwa mara baada ya mahojiano watuhumiwa ho walikiri kwamba walikuwa wamehifadhi bangi hiyo kwa ajili ya kuuza na mpaka hivi sasa jeshi la polisi limeshawafikisha watuhumiwa hao mahakamani

Post a Comment

0 Comments