Ticker

6/recent/ticker-posts

ISRAEL YATISHIA KUJENGA HEKALU NDANI YA AQSWA

Waziri wa Nyumba wa utawala wa Kizayuni wa Israel amesema kuwa, watajenga hekalu kwa ajili ya Mayahudi ndani ya ua wa msikiti Mtukufu wa al Aqswa. Uri Ariel ambaye ni mwanachama wa chama chenye misimamo mikali cha 'Jewish Home' amesema kwamba, Baraza la Mawaziri la Israel limesimamisha ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan lakini kwamba atahakikisha kuwa hekalu la Mayahudi linajengwa ndani ya Masjidul Aqswa.
Huku akitoa matamshi ya kufurutu ada na ya kibaguzi waziri huyo wa Israel sambamba na kubainisha kuwa, kuna matakwa ya kuundwa serikali mbili za Palestina na Israel amesema kwamba, njia pekee na ya uhakika eti ni kuwepo serikali moja tu ya Israel katika eneo hilo.
Inafaa kukumbusha hapa kuwa, viongozi wa utawala ghasibu wa Israel wanafanya kila njama ili waweze kuharibu athari na utambulisho wa Kiislamu na Kiarabu katika mji wa Quds kwa lengo la kuuyahudisha mji huo

Post a Comment

0 Comments