BREAKING NEWS

Thursday, March 27, 2014

CHEKA NAIROBI IMENIFANYA NIJIAMINI KATIKA MCHEZO WA NGUMI


Bondia Fracis Cheka amejigamba kambi aliyoweka jijini Nairobi nchini Kenya imemuongezea kujiamini kuelekea pambano lake la ubingwa wa dunia dhidi ya bondia valain ludov  kutoka Russia

Akizungumza na LIBENEKE LA KASKAZINI BLOG mjini hapa akiwa safarini kuelea Dar-es-saalam kutokea Nairobi cheka amesema kuwa kwa kuweka kambi Nairobi amejijenga kisaikolojia na pia mazoezi aliyoyapata kutoka kwa mabondia wa Kenya yamemuongezea mbinu hususani za kupambana na mabondia warefu.

“nimejifua kwa nguvu za kuongezewa mbinu na kocha wangu Abdala Salehe ‘comando’ mazingira yalikuwa mazuri nina kila sababu ya kujivunia mazoezi niliyopata nikiwa Nairobi”alisema Cheka.

Cheka alisema kuwa mabondia wengi wa Kenya ni warefu tofauti na wa Tanzania ambao wengi ni wafupi na hali ya hewa ya Nairobi ni nyepesi inayoruhusu kufanya mazoezi mazito na kwa muda mrefu na kwa sasa anajiona yuko tayari kumvaa mrusia huyo.

Cheka aliwahakikishia mashabiki wake na wadau wa ngumi hapa nchini kufanya vizuri katika pambano hilo hivyo wakae mkao wa kula kwani katika pambano hilo anatarajia kuiletea nchi yetu heshima kwa pambano la ngumi.

“Mashabiki wakae mkao wa kula na waje kuona namna ntakavyomchakaza huyo mrusia kwani najua kushinda kwangu kutailetea hata nchi yangu heshima na wadau wa ngumi watapata furaha kuona ushindi unabaki nyumbani” Alijitamba Cheka.

Pambano hili ka ubingwa wa dunia linalotambuliwa na IFB litafanyika jijini dare s salaam April 5 na maandalizi ya jumla kwa bondia Francis Cheka yamekamilika asilimia mia moja kama alivyoelezea.

Cheka aliyekuwa ameambatana na kocha wake Abdala Salehe ‘comando’ alipitia mkoani arusha ambapo alipumzika kwa muda mfupi kabla ya kuendelea na safari yake.

Cheka pia alibahatika kuona mazoezi ya mabondia wa mkoani Arusha ambao walikuwa wanafanya mazoezi kwenye uwanja wa kumbukumbu ya sheikh amri abeid mjini hapa.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates