BREAKING NEWS

Thursday, March 27, 2014

KAMPUNI YA KITAALII YA TANGANYIKA FILM YAKUSUDIA KUIMARISHA SEKTA YA MICHEZO SIHA


UONGOZI wa kampuni ya Utalii ya Tanganyika Film tawi la Ndarakwai Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro umesema kuwa umekusudia kuimarisha sekta ya michezo kwa lengo la kuwawezesha vijana katika  wilaya hiyo katika harakati za kuimarisha michezo.
 
Meneja wa Kampuni hiyo tawi la Ndarakwai, Thomas Olekuya alisema hayo wakati akizungumza na wachezaji wa timu ya Roseline FC na kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya michezo kwa la  kuimarisha michezo katika kata ya Ndumeti wilayani hapo kwenye kikao kilichofanyika kwenye uwanja wa shule ya  msingi Roseline.

 
Alisema, kampuni yake imeamua kuimarisha timu moja ya ndani ya kata hiyo  jambo ambalo litarahisisha hata upatikanaji wa vifaa na misaada kwa wepesi zaidi kuondoa tatizo sugu la upatikaji wa vifaa vya michezo
.
"Ndugu wachezaji wa  timu hii ya Roseline nawaahidi kuwa
nitahakikisha kwamba  Sekta ya Michezo inapata nguvu zaidi kutokana na umuhimu wake  uliojichomoza hivi karibuni wa kutoa ajira endapo Vijana hao watajituma vilivyo."alisema Olekuya
 
Alisema suala  la kuimarisha michezo  litakwenda sambamba na
upatikanaji wa vifaa vya michezo ikiwemo Mipira, Nyavu Magoli na Jezi ambapo alisema zimo ndani ya uwezo kampuni  kulingana na utaratibu aliouweka wa kusaidia vijana kupitia michezo
 
Akipokea  vifaa hivyo vya michezo kwa niaba ya wachezaji wa timu hiyo diwani wa kata ya Ndument , Charles Mwaijage aliishukuru kampuni hiyo kwa kuona umuhimu wa  kutatua changamoto zinazowakabili katika sekta ya michezo ikiwa ni pamoja na uhaba wa vifaa vya michezo ya aina mbalimbali
 
Diwani huyo alisema  kutatuliwa  kwa changamoto hizo kutawawezesha Vijana walio wengi wa jimbo hilo kuepuka kusambaratika pamoja na vishawishi vinavyoweza  kuwapelekea kujiingiza katika matendo maovu.
 
Hata hivyo Meneja huyo  alikabidhi seti ya Jezi, mpira,vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja  kwa timu hiyo pamojana kuwaahidi kuwapatia viatu kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali yatakayoanza wilayani hapo

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates