TUZO YA MWALIMU BORA ZAIDI DUNIANI YAZINDULIWA

Tuzo ya mwalimu bora zaidi duniani imezinduliwa.
Tuzo hiyo yenye thamani ya dola milioni moja, itakabidhiwa mwalimu ambaye anafanya kazi ya ualimu na ambaye atathibitisha kuwa mchango wake kwa jamii umekuwa bora zaidi kuliko walimu wengine wote duniani.
Pesa hizo zitatolewa kwa kipindi cha miaka kumi, lakini mwalimu huyo ataendelea kufundisha angalau kwa miaka mingine 5.
Tuzo hiyo ambayo imezinduliwa na wakfu wa Varkey Gems, shirika ambalo hutoa mchango mkubwa katika sekta ya elimu duniani, inaungwa mkono na mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid al Maktoum.
Mwenyekiti wa wakfu huo ni Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton. Bwana Clinton amesema kuwa ni muhimu sana kuwavutia watu bora zaidi kuwa walimu na pia kuwaza kuwathamini na kuthamini kazi zaO.
Unadhani mwalimu wako anaweza kushinda tuzo hii?

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia