BREAKING NEWS

Friday, March 28, 2014

MAMEYA NA WAKURUNZI TANZANIA WAKUTANA ARUSHA HII LEO

Mwenyekiti wa TACINE  Atanasi Kapunga akiongea katika mkutano huo
Mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela Akiwa anafungua rasmi mkutano wa umoja wa majiji  TACINE  uliofanyika jiji Arusdha hivi leo
washiriki wa  mkutano mkuu wa TACINE wakiwa wanamsikiliza mgeni rasmi akiwa anafungua mkutano

Wito umetolewa kwa Halimashauri zote nchini kutafuta njia mbadala za kuongezea Mapato yake ya ndani  tofauti na ilivyizoeleka kutegemea mapato yatokanayo na ushuru mbalimbali wanaokusanya katika halimashauri zao.
Wito huo umetolewa jana  na mkuu wa ya wilaya ya Arusha John Mongela wakati  akifungua mkutano mkuu wa    asasi ya umoja wa majiji Tanzania TACINE   inaowakutanisha  wakurugenzi pamoja na mameya wa majiji tanzania uliofanyika mkoani hapa.
Alibainisha kuwa  watendaji wa halimashauri  zote hapa nchini wanatakiwa kuangalia namna ya kuleta maendeleo katika halimshauri zao kwa kuunda miradi mikubwa  yenye tija  ambayo inaweza kukuza mapato ya halmashauri zao.
Alisema kuwa  inabidi halimashauri za majiji ziunde miradi   ambayo itasiaidia kuongeza ushuru mkubwa wa masoko wakati miradi hiyo kama ilivyo kuwa   awali  kwa halmashauri ya jiji la Arusha ilikuwa ikikusanya kiasi cha shilingi milioni  kumi ambapo kiasi hicho  kitasiaidia kwani kitaongezaka adi kufikia milioni ishirini.
Mongela alisema kuwa Halmashauri zina nafasi kubwa ya kufanya miradi mikubwa yenye tija na ambayo inaweza kuleta faida kubwa  na aendeleo makubwa.

Aidha aliwasihi wakurugenzi pamoja na mameya wote kujitaidi kutumia ipasavyo nafasi zao za ungozi haswa katika swala la kuwaletea wananchi maendeleo ili wakifikia  katika kipindi cha kustaafu au kupunzika katika nafasi zao za uongozi waache kitu hususa ni mradi ambao utakuwa  wa kihistoria.
“iwapo meya au mkurugenzi utafanya kitu  ambacho kitakuwa kizuri kama mradi ukifikia kipindi cha kustaafu au utakapo maliza kipindi chako  mradi ambao uliufungua kipindi cha   uongozi wako basi utanufaisha watu na utapata sifa kubwa ambayo aita saulika”alisema Mongela

Kwa upande wa  mwenyekiti wa   TACINE ambaye ni meya wa jiji la mbeya Atanasi Kapunga alisema kuwa dhamira kubwa ya umoja wao   kukutana katika jiji hili ni kuwaakikisha majiji yote yana kuwa na hadhi ya  inayo fanana .

Aliongeza kuwa pia  umoja huu unawezesha  majiji haya kuwa katika hali ya madhari nzuri pamoja na mpangilio uliomzuri ambao unahadhi ya jiji jambo ambalo litapelekea kuongezeka kwa vipato na maendeleo kwa wananchi.

Kwa upande wa meya wa shinyanga Gulamhafeez Mukadam alisema kuwa umoja  huu umesaidia mambo mengi ikiwa ni pamoja   na   kuleta maendeleo mbalimbali katika halimashauri mbalimbali.

Alitolea mfano bara bara za mijini ambazo zimejengwa katika halimashauri   mbalimbali alibainisha kuwa bila umoja huu wa majiji zisingewezwa kujengwa.
Alibainisha kuwa changamoto moja wapo wanaopata katika umoja huu ni pamoja na kukosa ushirikiano wa kutosha kutoka katika wizara zetu    jambo ambalo alibainisha kuwa ni changamoto kubwa inayowakabili hivyo aliiomba wizara husika ijitaidi kuwapa ushirikiano.

Pia  Mukadam aliwasihi viongozi mbalimbali wa halmashari za manispaa zote hapa nchini kuweka msimamo katika katika swala la kuleta maendeleo  na wasiangalie nyuma walipotoka bali waangalie mbali wanapokwenda na kitu kana watawafanyia wananchi nao wanufaike.


Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates