Ticker

6/recent/ticker-posts

SEIF AWATAKA WAKAZI WAKATA YA ELERAI KUHUBIRI AMANI NA KUWAKATA WOTE WASIOTAKA MANI



KATIBU mkuu wa CUF na makam wa kwanza wa raisi wa serekali ya mapinduzi ya Zanzibar Maalimu Seif Sharif Hamad akimuombea kura mgombea wa udiwani wa kata ya Elerai John Gilbert Bayo kwa wakazi wa kata hiyo kwenye viwanja vya shule ya msingi Elerai na kuwataka kumchagua mgombea
Wakazi wa kata ya Elerai wametakiwa kuhubiri amani na mshikamano na kukataa wale wote ambao hawaitakii amani Mkoa wa Arusha kwani wamekuwa wakiwaumiza kiuchumi na kimaendeleo na kuwa vurugu na maandamano kwao hayana tija badala yake ni hasara kwa uchumi na maendeleo ya mkoa wao.

Kauli hiyo imetolewa na makamu wa kwanza wa serekali ya umoja wa kitaifa(SMZ)Maalim Seif Sharif Hamad wakati akiongea na wakazi wa kata hiyo alipokuwa mgeni rasmi kwenye kampeni za uchaguzi wa kata hiyo.

Sharif hamad aliwataka watanzania kutobaguana kwa visingizio vya ukabila udini na aina yeyote ya ubaguzi kwa minajili ya kuvurga amani na mshikamano wa taifa letu na kuwa siasa ni maisha ya watanzania wote hivyo kila mmoja wetu anawajibu wa kutunza amani na mshikamano sanjari na kuacha ushabiki kwenye siasa.

“Ndugu zangu wana Arusha siasa ndiyo maisha yetu na vijana ndio msingi wa taifa kwani ndiyo nguvu kazi sasa hawa wakitumika vibaya kwa maslahi ya wachache kufanya vurugu na maandamano tutakuwa tunaelekea wapi”alihoji Maalim Seif.

Makamu huyo alisema watanzania wote bila kujali rangi,ukabila,na udini wanahaki sawa za kupata mgawanyo wa kiuchumi hapa hakuna ambaye hana hati miliki na nchi hii kwani nchi hii ni yetu sote bila kujali itikadi za vyama.

Alisema anashangaa kuona nchi hii yenye rasilimali lukuki na ardhi isiyokataa mazao yeyote hapa dunia ikiwa katika hali mbaya ya kukosa chakula wakati imejaaliwa neema kubwa hii ndiyo sera za chama cha mapinduzi kilipotufikisha  na kuwataka watanzania kuacha ushabiki wa kisiasa na kujiuliza tumekosea wapi ilituweze kuyapatia majibu sahihi jmatatizo yetu.

Post a Comment

0 Comments