KONGO YAAZIMIA KUKABILIANA NA M23



Serikali ya Jamhuri ya Kidomekrasia ya Kongo imetangaza kuwa itakabiliana vilivyo na vitisho vya waasi wa M23 nchini humo. Lambart Mende msemaji wa serikali ya Kongo DRC jana alitangaza kuwa, serikali ya Kinshasa inavizingatia vitsho vya waasi wa M 23 hasa baada ya waasi hao kuuteka tena mji wa Goma, ambao ni makao makuu ya mkoa wa Kivu Kaskazini.
Msemaji huyo wa serikali ya Kongo ameongeza kwamba, suluhisho pekee kwa waasi hao ni kuendelea na mazungumzo ya kusaka amani huko Kampala Uganda na kuwatahadharisha kuwa, vikosi vya Umoja wa Mataifa viko katika eneo la Mashariki ya Kongo ambako vinashirikiana na wanajeshi wa Kongo, hivyo ni bora M23 waache machafuko.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post