Watu watatu wauawa na jeshi Misri

Maafisa wa usalama mjini Cairo, Misri leo wamewaua kiasi ya waandamanaji watatu baada ya mamia ya waandamanaji hao waliojitokeza kumuunga mkono Rais aliyeng'olewa madarakani Mohammed Mursi kuanza kuelekea katika kambi ya kijeshi mjini humo ambako kiongozi huyo anazuiliwa na wanajeshi waliompindua.Maelfu ya wafuasi wa Mursi wameandamana katika miji kadhaa nchini humo kwa kile udugu wa kiislamu umekiita 'Ijumaa ya ghadahabu' kutokana na mapinduzi ya kiongozi wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia mwaka mmoja uliopita.Mtu aliyeshuhudia ameliambia shirika la habari la Reuters aliwaona watu kadhaa  wakiwa na majeraha ya risasi.Maelfu ya watu pia waliandamana mijini Alexandria na Assiut kupinga serikali ya muda iliyoapishwa jana.Mjini Ismailia wanajeshi walifyatua risasi hewani wakati wafuasi wa Mursi walipojaribu kuingia katika ofisi ya gavana wa jimbo hilo.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post