Ticker

6/recent/ticker-posts

TANAPA WAZINDUA KAMPENI YA KUTANGAZA UTALII WA NDANI JIJINI MWANZA.

Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu akiwasili katika viwanja vya Yatch Club jijini Mwanza kwa ajili ya shughuli ya uzinduzi wa kampeni ya kutangaza Utalii wa Ndani.
Baadhi ya Waaandishi wa Habari waliofika kwa ajili ya shughuli hiyo ya uzinduzi wa kampeni ya kutangaza Utalii wa ndani.
Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Hifadhi za Taifa wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya kutangaza Utalii wa ndani.
Kikundi cha Ngoma cha Bujorwa kikitoa burudani kwa wageni waalikwa.
Meneja Mauzo wa Kampuni ya Tigo mkoa wa Mwanza Kassim Azizi (kushoto) akiwa na Meneja Msimamizi wa wateja wa makampuni Issa Orry  katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya kutangaza Utalii wa Ndani iliozinduliwa jijini Mwanza.
Wacheza ngoma wa kikundi cha Bujorwa cha jijini Mwanza wakitoa burudani mbele ya mgeni rasmi ,Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kutangaza Utalii wa Ndani.
Mkurugenzi wa Idara ya Utalii wa Shirika la Hifadhi za Taifa ,Tanzania (TANAPA) Ibrahim Musa akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Yatch club.
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii,Tanzania ,Devotha Mdachi akizungumza katika hafla hiyo.
Baadhi ya Wahariri na waandishi wa habari waliofika katika hafla hiyo.

Post a Comment

0 Comments