Ticker

6/recent/ticker-posts

TFDA KANDA YA KASKAZINI LAFUNGA GHALA LA VIPODOZI BANDIA

Mamlaka ya chakula na dawa kanda ya kaskazini TFDA, imefunga ghala la vipodozi bandia(feki) lililoko mafichoni katikati ya makazi ya watu jijini Arusha,na kisha kuteketeza shehena hiyo ya vipodozi hivyo.

 Mamlaka ya chakula na dawa ilifanya ukaguzi  wa kushutukiza,na kukuta limesheheni ghala hilo limesheheni vipodozi bandia   vilivyopigwa marufuku kuingizwa nchini.

Ukaguzi huo wa kushutukiza umefanyika juzi Januari 14,baada ya mamalaka ya chakula na dawa TFDA, kupata taarifa za siri za kuwepo ghala la vipodozi bandia kwenye makazi ya watu eneo la mita 200 jijini Arusha.

Akizungumza wakati wa zoezi la kuteketeza bidhaa hizo kwenye Jalala kuu la halmashauri ya jiji la Arusha, lililopo eneo la Mriet kata ya Sokon one ,meneja wa TFDA, kanda ya kaskazini Damas Matiko, amesema bidhaa hizo ambazo zina thamani ya shilingi milioni 7 zilizoteketezwa hazikusajiliwa kwa soko la Tanzania.

Zoezio hilo la kufunga ghala hilo limefanyika chini ya ulinzi wa jeshi la polisi  baada ya TFDA,kupata taarifa za siri na hivyo kunyata na kulikuta ghala hilo likiwa na bidhaa hizo zenye uzito wa tani 2  ambazo ni vipodozi vilivyopigwa marufuku kuingizwa nchini na katika  upekuzi huo kulikutwa shehena hiyo ya   bidhaa hizo zisizofaa kwa matumizi ya binadamu .

Matiko , amesema kuwa ghala hilo limekutwa mafichoni eneo la mita 200 kwenye makazi ya watu katika jiji la Arusha, ambapo bila taarifa sahihi huwezi kufahamu kama kuna ghala tena lililosheheni vipodozi  .

Amesema ghala hilo lipo kwenye nyumba ya mtu ambapo hutumika kuhifadhia bidhaa hizo za vipodozi, ambapo huwa inahamishwa kidogo kidogo kupelekwa kwenye maduka kulingana na mahitaji .

Matiko,amesemja TFDA, itaendelea kusimamia utekelezaji wa lengo lake  la kulinda na kuokoa afya za walaji ili kuwaepusha kupata maladhi mbalimbali yakiwemo kansa, athari za ngozi, mwili, viungo vya uzazi mfumo wa damu kuathiri ubongo na makuzi ya watoto.

Ameongeza kuwa lengo lingine la TFDA ni kuondoa bidhaa zote ambazo hazikusajiliwa kwa soko la Tanzania kwenye maduka ili ibakie bidhaa zinazotakiwa tu .


Amesisitiza kuwa ni lazima wafanyabiashara wafuate taratibu kwa kuingiza bidhaa zinazoruhusiwa kwa soko la ndani ambazo zimesajiliwa na TFDA ,ambazo lugha na maelezo yake ni ya Kiingereza na kiswahili tu, na si vinginevyo.

Kwa upande wake Afisa afya kutoka jiji la Arusha, Angela Mogitu, amewatahadharisha wanawake kuepuka kutumia vipodozi ambavyo hawavifahamu  kwa kuwa vinawasababishia madhara makubwa .

Mogitu, amesema vipodozi vyote vilivyopigwa marufuku vina madini ya Zebaki ambayo ni hatari kwa afya ya mtumiaji  pia huharibu mfumo wa uzazi na damu  na ngozi hivyo wasivitumie madhara yake ni makubwa.

Mimiliki wa ghala hilo,Deo Simon Mwacha  (32)ambae pia anamiliki duka la kuuza vipodozi katika mtaa wa Mnazi mmoja jijini Arusaha, amekiri kuingiza bidhaa hizo na kudai kuwa huwa ananunua katika maduka makubwa ya vipodozi jijini Dar es Salaam.

Macha amesema amekuwa hununua vipodozi hivyo na kuviuza kwa wateja mbalimbali dukani kwake lakini  hakujua kama vina madhara .

Mara baada ya kutiwa nguvuni mtuhumiwa huyo akiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi alipakia bidhaa zake kwenye gari lake Toyota Noah,hadi jalala kuu la Arusha lililopo eneo la Mriet kata ya sokon one na kuishusha kisha akishuhudia ikiteketezwa kwa moto na mamlaka ya chakula na dawa TFDA.
 
 

Post a Comment

0 Comments