Ticker

6/recent/ticker-posts

CHADEMA KANDA YA KASKAZINI WALIA NA UCHELEWESHWAJI WA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA



 Mwenyekiti wa chadema mkoa ambaye pia ni katibu wa taifa wa chadema kanda ya kaskazini akiongea na waandishi wa habari hii leo ndani ya ofisi za chama hicho kanda zilizopo ndani ya jiji la Arusha
 waandishi wa habari wakiwa wanasubiri mkutano wa chadema uanze









 naibu meye wa jiji la Arusha Prosper Msofe akiwa anafafanua jambo mbele ya waandishi wa habari
Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa, amesema wanaotaka kutangaza nia ya kuwania ubunge katika majimbo ambayo tayari yana wabunge wa chama hicho, wanatakiwa kusubiri hadi Bunge litakapovunjwa Julai 2, mwaka huu, ili kuwapa wabunge waliopo nafasi ya utulivu kufanya kazi za kibunge.
 
Alisema hadi sasa hakuna mgombea wa kiti cha ubunge Jimbo la Arusha, ambaye ameandika rasmi barua ya kuelezea nia yake ya kugombea ubunge katika jimbo hilo.
 
Alisema kwa mujibu wa utaratibu waliojiwekea, Ofisi ya Kanda ndiyo yenye jukumu na wajibu wa kuratibu mchakato wa kupokea barua rasmi pamoja na wasifu wa wagombea.
 
Hata hivyo, alisema mbunge wa sasa, Godbless Lema ameonyesha nia ya kuendelea kugombea tena kiti chake.
 
Alisema utaratibu waliojiwekea kwa majimbo ambayo yana wabunge wa chama hicho, ni kwa wagombea wanaotaka kutangaza nia kusubiri hadi bunge litakapovunjwa Julai 2, mwaka huu.
 
“Najua wapo wanachama wenye nia ya kugombea ubunge, lakini bado hawajaandika barua rasmi kuomba, inawezekana wametangaza nia zao huko mitaani na kwenye redio, lakini hawajafanya hivyo kwa kuleta barua rasmi ofisini, utaratibu wetu kwenye majimbo yenye wabunge, wasubiri hadi bunge litakapovunjwa,” alisema na kuongeza hawatakiwi kutangaza hadharani ila kwa kupeleka barua rasmi ofisini.

Post a Comment

0 Comments