Ticker

6/recent/ticker-posts

MAKAMU MWENYEKITI WA UMOJA WA WATANZANIA UJERUMANI KUWASILI NCHINI LEO

 Makamo mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania  Ujerumani UTU e.V  Mheshimiwa Peter Kazaura

Makamo mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania  Ujerumani UTU e.V  Mheshimiwa Peter Kazaura kuwasili nchini Tanzania leo 02.02.2015 kwa ajili ya kufanya mazungumzo na kiongozi wa juu wa Taifa. akiwa Tanzania atafanya mazungumzo na uongozi wa mashirika  yafuatayo TIC, Basata, Wizara ya Ardhi, NSSF, NHC,  Tanzania Diaspora Initiative na Wizara ya Utamaduni Michezo na Vijana.
 Mazungumzo hayo yatalenga upatikanaji wa Fursa zilizopo Tanzania kwa Diaspora. akiendelea kueleza msemaji wa Umoja huo Watanzania wanaoishi ujerumani wangependa pia kuhusishwa kikamilifu katika shughuli za maendeleo nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na Afya, Elimu. 

naye  Mwenyekiti wa  Umoja huo Mhe. Mfundo Peter Mfundo alithibitisha kuwepo kwa safari ya Makamo Mwenyekiti Mhe Peter Kazaura na  alisema  UTU e.V umechukua uamuzi huo  baada ya Watanzania nchini Ujerumani kukosa nafasi ya kuongea na Rais wa Tanzania  wakati wa ziara ya Rais nchini Ujerumani.
Pia watanzania wanaoishi ujerumani wanaulalamikia ubalozi kuwa viongozi wa umoja wao walinyimwa nafasi ya kuonana na kumsalimia Mhe.Rais Dkt.Jakaya Kikwete.

Post a Comment

0 Comments