Ticker

6/recent/ticker-posts

HAYA NI MAPOLISI AU MAJAMBAZI`

 
Hemed Kivuyo.
 
Pamoja na mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Said Mwema kuonyesha jitihada za makusudi za kulitakasa jeshi hilo na kurudi katika kulinda usalama wa Raia na mali zake,badi jitihada hizo zinaonekana kuwa siyo lolote siyo chochote.
 
Mbio ndefu za IGP zinavutwa shati na kurudi nyuma na baadhi ya askari wasiyo waadilifu na hivyo kushindanisha mbio zao dhidi ya mbio za kamanda Mwema.

IGP Said Mwema alipoingia katika cheo hicho alijinasibu mambo mengi ikiwa ni pamoja na `kujidai` kuwa jeshi lake litaenda kisomi,aliwataka wananchi kusahau yote yaliyopita na kushirikiana na jeshi hilo katika kutokomeza uhalifu wa aina yeyote.

Mimi ni mmoja kati ya waumini wazuri wa kauli zako nzuri,lakini kadiri siku zinavyokwenda nakatishwa tamaa na baadhi ya askari wako ambao sioni sababu ya kutokuwaita `wahuni` hao baadhi ya Askari wako .

Pamoja na kali za IGP bado baadhi ya polisi wanashiriki katika vitendo vua uhalifu,bado wanapiga raia risasi hovyo,bado wanapokea rushwa kwa kasi,hili ni jeshi la kisomi?
 
Inanitisha kuamini kama kweli polisi wanaokabidhiwa silaha za moto kama wana akili timamu achilia mbali elimu.Hiingii akilini kuona askari akifyatua risasi hovyohovyo tena kwa mwananchi asiyekuwa na silaha ya moto,huyu Askari kaenda chuo gani? Huyu Askari gani anafika malai na kuanza kufuatua risasi kama `majununi` bila kwenda kisomi na kubaini mtandao wa uhalifu na kukamata wahalifu ili kubaini wengine? 

Polisi wasomi na wanaofanya kazi kwa ustadi wa hali ya juu na usomi’siyo tu wameendelea kuuwa raia wasiyokuwa na hatia kwakuwafyatulia risasi bali wameendelea  kudhihirisha `upofu wao wa akili` kwakuingia katika nyumba ya mtu asiyekuwa mwalifu na kumpiga Risasi begani.( hao ndiyo polisi wasomi)

Mwandishi wa habari amepigwa Risasi begani na Askari baada ya kumwingilia ndani kwake,na kwa mujibu wa polisi,wanadai walielekezwa kwa Mama mmoja ambaye anahisiwa kuwa mwalifu na hata kuhifadhi wahalifu.

Intelejensia ya Polisi imeshindwa kubaini mtandao wa wahalifu? Mmeweza kubaini maandamano yasiyo halali tu.`polisi dhaifu`.

Matukio ya kutisha naya kuogofya yanayofanywa na baadhi ya askari katika vituo vya polisi bado zinarudisha nyuma jitihada za Mwema za kutaka wananchi kuonyesha ushirikiano kwa jeshi hilo ili liweze kukabiliana na uhalifu wa aina mbalimbali.  
 
Kutokana na baadhi ya askari kukiuka maadili yao na sasa kunatafsirika kuwa hukumu ipo mikononi mwao na kituo cha polisi siyo tena mahali salama kama ilivyokuwa ikitamkwa hapo awali.
 
Miaka mitatu iliyopita Jijini Arusha vija wawili waliuawa na polisi huku jeshi hilo likijitetea kuwa watu hao ni majambazi waliyotaka kuvamia kituo kimoja cha mafuta ,na baada ya kuundwa tuma ilibainika watu hao siyo majambazi kama polisi ilivyojinasibu. (Polisi dhaifu) ``wamebaki kula rushwa``.
 
Mpaka sasa haifahamiki polisi hao wapo wapi na wanafanya nini ,lakini roho za watanzania hao zilipotezwa na polisi hao na kuliachia doa.
 
Jijini Dar es salaam siyo mara moja lakini hivi karibuni dereva tax mmoja alidaiwa kufa akiwa mokononi mwa polisi na kifo hicho kilitokea baada ya kuhojiwa kwa saa kadhaa na kuteswa.
 
Siyo hayo tu kuna matukio mengi ambayo yanadhihirisha kuwa jeshi hilo linapaswa kujitofautisha na majangili ambayo huwavamia rai wema na kuwapora na hata kuwaua,wakati mwingine jambazi anaweza kukuingilia kwako akakubia na kukuachia roho yako,iweje polisi waingine na kuua ama kujeruhi? Tuogope polisi kuliko majambazi?
`polisi dhaifu` wanaongozwa na fikra mgando.
 
Kama itatokea majambazi yanavamia wananchi na kuwapora kisha kuwaachia roho zao zikiwa salama ,basi kuna kila dalili kuwa wananchi watapoteza imani na polisi ambao hawapori mali zao ila wanafisidi roho zao. Matumaini hayo yanakuja  baada kukutana na kauli inayosema `` mali inatafutwa na kupatikana lakini siyo roho``
 
 
Baadhi ya skari kutoa lugha chafu katika vituo vya polisi,kuwatesa watuhumiwa na kufanya wanalotaka kwa mtuhumiwa na hata wana ndugu waliofika kujua kinagaubaga juu ya ndugu yao kushikiliwa ,ni jambo linaloleta ukakasi katika masikio ya kila anayejua maana ya jeshi hilo na sheria za nchi.``polisi wanaishi na fikra zilizokufa``
 
Polisi bado wanafanya matukio ya kudhalilisha raia wema wanaotuhumiwa na hata kuwabambikia tuhuma .``jeshi la polisi limekosa weledi``.
 
Hali ya wananchi kuteswa,kutolewa maneno ya lugha chafu,kubambikiwa kesi na hata kupotezewa maisha wakiwa katika vituo vya polisi kama ilivyotokea siku za karibuni,inazidi kuifanya jamii ipoteze imani na jeshi hilo na hata IGP Mwema mwenyewe ambaye anapaswa kuonyesha jitihaza za kuondokana na hilo kwa vitendo na kwa matukio hayo mpaka sasa IGP MWEMA unapaswa kuachia ngazi na ukafanye shughuli nyingine. `haiingii akilini kwa polisi aliytoka chuo kwenda kinyume na maadili kupitiliza alafu jeshi likakaa kimya..`Abadan`

IGP kuna madhambi mengi yanafanywa na baadhi ya polisi wako ,wewe huwezi kuwajua ,sisi tunawajua na kuwaona huku mitaani/kuna asakri mmoja (trafiki) mmempa pikipiki kama unahitaji jina lake ntakupa,sina hakika na kiwango chake cha elimu lakini nachoweza kusema kwa lugha nyepsi kuwa Askari huyu ni kielelezo cha `upuuzi` wa baadhi ya Askari ndani ya jeshi hilo.

Pamoja na ujana wake unaomwezesha kufanya kazi kwa bidii na kufuata maadili,lakini amekuwa kama ameingiwa `maruhani` ya kupokea rushwa na `uzinzi`

Ndiyo jamii ya walewale waliyomfyatulia Risasi Mwandishi,sisitaji kutafuta Kiswahili kingine zaidi ya `wahuni` wachcahe ndani ya jeshi la polisi.
 
Ninaposema hivyo namaanisha kuwa IGP Mwema ana wajibu na anapaswa kuwajibika,kwanini Askari wanaingia nyumba ambayo hawakuelezwa? Wamesomea wapi? Kwanini aingie na kufyatua risasi? Alikuwa anakabailiana na wanamgambo wa `TALIBANI? Aliingia katika kambi ya M23? Aliingia katika mapango ya Torabora? Tulitaka kuporwa ziwa nyasa? ``Huu ni upuuzi`` hatupaswi kukaa kimya likapta hivihivi  ni lazima IGP MWEMA awajibike kwakuwa siyo tukio la kwanza Jeshi lake kwenda kinyume na maadili ya jeshi la hata katiba ya Nchi.
  
 Mpaka sasa pamoja na jitihada za wakuu mbalimbaliu wa jeshi hilo bado polisi wanahusika na kupoteza maisha ya raia wema wanapokuwa chini ya himaya yao ,jambo ambalo linaweza kusababisha machafuko kama wananci nao wataishiwa uvumilivu.
 
Imani iliyoanza kurejea kwa wananchi dhidi ya jeshi hilo  inaanza kutoweka siku hadi siku hasa kutokana na  vitendo viovu vya baadhi ya polisi ambao hatuoni hatua zozote wanazochukuliwa.
 
 
Askari `mkora` na `muhuni `atafanyakazi hiyo kihuni na kikora kisha kusababisha maisha ya wananchi kupotea  kama ilivyo hivi sasa.Suala la wananchi ambao  wanapelekwa katika vituo vya polisi  na baadaye kutolewa taarifa za kupoteza maisha siyo suala la mzaha kama polisi wanavyolichukulia kutokana na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria . `IGP NAKUHESHIMU..NAOMBA UONDOKE TAFADHALI..
 
Nasema hivyo kutokana na hatua zisizoridhisha ambazo polisi inachukua kwa waajiriwa wake pindi wanapofanya makosa kama hayo na hivyo kuzidi kuongeza idadi ya matukio kama hayo. KWANINI? IGP NAKUHESHIMU SANA ,NAKUPENDA ,NAPENDA UTENDAJI WAKO ILA HAPA TULIPOFIKA  NAOMBA UTAFUTE KAZI NYINGINE TAFADHALI…MUOMBE RADHI AMIRI JESHI MKUU KISHA UMUOMBE KUACHIA NGAZI..NIPO TAYARI KUKUSAIDIA KUOMBA HILO KWA RAIS WETU MSIKIVU.
 
Toka awali jeshi hilo linafanya makosa katika kuajiri vijana ambao hukaa katika mafunzo ya muda mfupi ambayo ni ya miezo sita kisha kupelekwa mikoani ,tayari kwakuanza kazi na hapohapo hujifunza kazi kwakuwakamata vijana katika miji mbalimbali ili kupata uzoefu wa kazi.
 
Kama kijana alilelewa nyumbani  kwao na akawa ni `mvuta`bangi`asiyekuwa na heshima kwa mkubwa wala mdogo ,akawa ni mwenye kutoa maneno yenye lugha chafu na sugu wa tabia mbovu ,sidhani kama miezi sita inaweza kubadilisha tabia yake ya uvutaji bangi na kutoa maneno yenye ukakasi kwa jamii alafu tukategemea miezi sita itarekebisha tabia yake chafu.
 
Na ndiyo maana kuna baadhi askari ambayo hukaa katika vituo vya polisi lakini ni watumiaji wa mihadarati ,ni wasiyo na heshima na wenye kutoa lugha chafu kwa raia waliyostaarabika.
 
Haishangazi sana kusikia polisi wameshiriki kupoteza maisha ya raia mwema aliyefikishwa kituoni kwa kosa la ajabuajabu lisilo na kichwa wala miguu.
 
 `.
Wananchi hawa hawa wa Tanzania wanateswa na wahalifu ,wanateswa na umasikini,wanateswa na ahadi zisizotekelezeka zinazotolewa na wanasiasa na bado pia wateswe na polisi ! Sasa watanzania watakosa pakukimbilia pamoja na amani iliyopo .
 
Amani bila kuwepo amani ndania ya mikono inayoitwa salama ya jeshi la polisi siyo amani timilifu.
  Watanzania wana moyo hawana jiwe,mengine wapunguziwe
Abadana, tusiwaache polisi wacheze na maisha ya raia wema watakavyo.IGP Mwema sasa uachie ngazi kwa kuhifadhi heshima
yako. KWA MUSTAKBALI HUU SIYO SABABU YA ASKARI HAO WACHCAHE KUENDELEA KULITUMIKIA JESHI LA POLISI,HAO SIYO POLISI BALI NI MAJAMBAZI”


0752 250157.

Post a Comment

0 Comments