WEZI WA NYAYA ZA TANESCO ZA SHABA WAKAMATWA ARUSHA


watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi  wamekamatwa na wananchi  baada ya kuwashika wakijaribu kutorosha zaidi ya mita 500 za yaya za shaba walizokata kwenye laini ya umeme  ya Usa feeder iliyopo wilayani Arumeru Mkoani Arusha.


Akizungumzia kutoea kwa tukio hilo tukio  meneja wa Tanesco mkoa  Engineer Nicholaus  Kamoleka alisema kuwa tukio hilo  lilitokea mwishoni mwa wiki  eneo la  Kikatiti Wilaya ya Arumeru, kwa Mangasha.

Adha alibainisha kuwa siku ya tukio  watu hao walikamatwa na  Wananchi  wenye hasira kali kwa kushiriana wafanyakazi watanesco  na   walikamatwa kuwa ni pamoja na  William Jonas (20), Hussein Abubakar (19), na Luwaich August (23) wote wakazi wa Daraja mbili Unga Ltd.


Aidha alibainisha kuwa baada ya umeme kukatika saa 8.30 usiku, ushirikiano kati ya wafanyakazi wa kituo cha TANESCO  Usa river na viongozi wa kijiji cha Kwa mangasha ndio uliweza kuwasiliana na kufuatilia swala hili ndipo walipowakuta watuhumiwa hawa na  kukamatwa.

 Kamoleka alisema kuwa tukio hilo la wizi limesababisha Tanesco  hasara ya Shilingi Millioni Ishirini na liliathiri mikoa miwili,mbapo alibainisha kuwa  wateja wa Wilaya nzima ya Arumeru Mkoani Arusha  na pia Wilaya nzima ya Hai mkoani Kilimanjaro walikaa bila umeme kwa masaa 12, kuanzia saa nane usiku hadi saa nane mchana.

Alisemakuwa  Watuhumiwa hao  wako chini ya ulinzi wa Polisi na uchunguzi unaendelea huku akibainisha kuwa Baada ya matukio ya wizi wa nyaya za shaba kuwa mengi katika laini ya umeme kubwa ya Usa river,Idara ya Usalama ya TANESCO Arusha ulimeanza kuzunguka na kuelimisha wananchi wa maeneo umeme unapopita na vijiji vya karibu kuwa ni   jukumu lao katika kulinda miundo mbinu, pia  imeanzisha  mfumo wa ulinzi shirikishi ambao umesha fanikisha kukamatwa watuhumiwa wanne hadi sasa.

Kamoleka aliwataka wananchi wa mkoa mzima wa arusha kuwa makini na kuendelea kutoa ushirikiano kwa tanesco kwa kuwafichua watu wote ambao wamekuwa wanafanya kazi yakuina nyaya za shaba pamoja na kuwafichua vishoka wote na wale watu ambao wamejiunganishia umeme bila kufuata utaratibu wa tanesco

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post