TBL YASHINDA RUFAA YA KUTOLIPA SBL

KAMPUNI ya Bia Tanzania Breweries  Limited (TBL),   imeshinda kesi inayohusisha  malipo ya Sh25 bilioni  dhidi ya Kampuni  ya Serengeti Breweries Limited (SBL) katika hukumu iliyotolewa na Baraza la Ushindani nchini (FCT).
Tume ya Ushindani nchini, mwaka 2010 iliitoza faini  ya asilimia tano ya mauzo TBL, kwa kujihusisha na tabia kinzani za ushindani wa biashara dhidi ya (SBL), asilimia hiyo inafikia takriban Sh25 bilioni.
Kutokana na uamuzi huo, TBL kupitia mawakili wake ambao ni Dk Ringo Tenga na Fayaz Bhojan walikata rufani.
Katika rufani hiyo, mawakili hao wa TBL waliwasilisha hoja mbalimbali, ikiwamo ya  FCC  haikuundwa ipasavyo kwa mujibu wa sheria na kwamba   mwenyekiti wake, Nikubuka Shimwela hakuteuliwa kama inavyostahili.
Mawakili hao waliendelea kudai kuwa, Mwenyekiti huyo aliteuliwa na Waziri wa Biashara siyo Rais wa nchi  kama sheria ya ushindani  inavyoelekeza, hivyo kufanya uamuzi uliotolewa  kuwa batili na unastahili kufutwa.
Licha ya hoja hizo, mawakili  hao wa TBL pia walidai kuwa, Mkurugenzi  huyo wa FCC naye hakuteuliwa kihalali.
Jopo la watu watatu, lililoongozwa na Jaji wa Mahakama Kuu, Razia Sheikh  lilisikiliza rufani na kukubaliana kuwa FCC  kwa kipindi hicho haikuwa imeundwa kwa mujibu wa sheria, hivyo  uamuzi wa TBL kutoa faini hiyo haukuwa halali.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia